Wanasiasa na viongozi wanapoamua kutunushiana misuli inayoumia ni demokrasia na sisi wananchi. Tujifunze kuachiana nafasi kila mtu afanye yake. Sisi watanzania, hatutaki kurudi kule tulikotoka. Tunatamani, tuishi kwa amani na uhuru wa kufanya yale tuliyo na haki nayo.
Mh Rais
@SuluhuSamia
umekiri kuwa hali ya kiuchumi si nzuri sana. Nikuombe sana, punguzeni sherehe za serikali. Kila siku aidha kuna uzinduzi, mkutano, etc. Mnapotwambia hali ni ngumu tuanze kuiona na kwenu. Hizi flash and shiny events zipunguzwe ili mtupunzuzie mzigo wa kodi.
Kwakuwa mgombea uraisi wa chama tawala amesema kuwa majimbo yatakayochagua upinzani hayataletewa maendeleo. Basi wananchi wa majimbo hayo wasitozwe kodi yoyote, au kodi zao zisipelekwe serikali kuu - wajiletee maendeleo yao. Kuwatoza kodi na kutowaletea maendeleo ni unyanganyi.
Mwenyekiti
@MagufuliJP
kura za maoni zimeonyesha dhahiri kuwa wana CCM wenzio hawakupendezwa na ununuzi wa wabunge wa upinzani, wamehadhirika vibaya.
Kimsingi mchakato ndani ya chama ulikuwa wa uwazi, tunatumai utaratibu huu mwema utafanyika pia October 2020 Watanzania waamue.
Dada yangu
@umwalimu
tumekulalamiakia weeeeeeeeeee na pengine mpaka kukunanga. Tusamehe mwaya.
You know what, take a day off... nami ntakuletea mkate wa kumimina, choroko za maua, samaki wa kupaka na uji wa bada uftarie.
Hakuna namna utafanya... we know now.
Ndugu zangu mkiamka muangalie hii interview ya Jenerali Mabeyo akisimulia yote yaliyojiri siku Rais Magufuli alivyofariki mpaka Rais Samia alivyopishwa. Nimejifunza mengi sana.
Huwa nina kawaida ya kununua umeme kila mwezi kwa kiwango kile kile bila kujali umekwisha au la na kuwapa watoto waweke. Leo nachungulia muamala wa unit, kumbe niko sorted kwa miezi kadhaa.
Somo, usisubiri umeme ukatike ndio ununue, wewe nunua tu, hauchachi!
Nimekuwa natamani sana kuuliza hili swali ila nasita, leo ngojea niulize.
Eti Hospital ya Mzena iko wapi? Na Je ni kwa ajili ya viongozi tu au hata sie Twaweza kutibiwa?
Labda sasa ni muda muafaka kujadili hili swala la harusi!
Mie naona maharusi wawajibike kugharamia harusi zao kwa uwezo wao. Michango ife.
Pili haya mashindano ya nani kafanya Harusi ya mamilioni mangapi, yanaleta stress na umaskini kwa fahari ya muda mfupi.
Nilipokuwa mdada, nilikuwa nalipa on first date kwa sababu
1. Nichague eneo na muda - kwa usalama wangu
2. Niwe na uhuru wa kuwa mimi
3. Niwe na control ya maongezi
4. Niondoke muda ninaotaka mimi.
5. Tusichukuliane poa
Nimeshtushwa na taarifa za kifo cha Rais wa Burundi, Mhe. Pierre Nkurunziza. Nitamkumbuka kwa uongozi wake imara na juhudi zake za kupigania amani, maendeleo na kuruhusu demokrasia. Kwa niaba ya Serikali na Watanzania nawapa pole familia na Warundi wote. Mungu amweke mahali pema.
Kura 9,953 zimepigwa na chama tawala kimeibua na ushindi wa asilimia 73 (73%). Nawapongeza sana. Nahisi hii ni poll pekee ya twitter walioshindwa kwa kishindo.
Hali ya vivukio aka flyover - kibongobongo
Dizaini kama Sir God yuko upande wetu hivi! Mana huu ufunuo wa leo lazima utuletee uzima wa milele.
#PigaKura
#KuraYakoMaishaYako
Kenya imefunga mipaka yake yote na Tanzania, itaruhusu tu mizigo kupita, na wanaopitisha mizigo wataruhusiwa tu pale ambapo vipimo vyao vya korona vitakuwa hasi (negative)
Tusipojifungia
Tutafungiwa.
Leo nimeenda kule nilikoanzia maisha, hizi ndio biashara zangu za kwa kwanza nilipokuja Dar -Mbagala (saloon na duka la mangi) Nilipokuwa Kilwa nilikuwa na goli la mitumba. Maisha ni hatua, Maisha ni safari
Kwakuwa Ikulu ya DSM sasa haitumiki kwa shughuli za kiserikali, na kwa kuwa siku za hivi karibuni iliongezewa wanyama wa aina mbalimbali. Napendekeza, Wasanii waruhusiwe kukodi na kutumia jumba hilo kwa shughuli zao za sanaa au liwekwe kwenye Airbnb.
Tutapata mapato yakutosha.
Kaka zangu na dada zangu naomba kujifunza kutoka kwenu. Husband material ana sifa gani? Kwa lugha nyingine nitajuaje kuwa mtu wangu ni husband material?
Wapinzani wanafanya siasa katika mazingira magumu sana. Ni wajibu wetu kuwachingia na kuwatia moyo.
Mimi nawachangia wagombea wanawake wa upinzani, hasa wale wanaogombea kwa mara ya kwanza, siwezi nikawa nahubiri ushiriki wa wanawake na sifanyi wajibu wangu
#Changia
hata 500
Nisiposema hili sitalala vema
So you know maumbile ya kike ni elastic, sasa huko kukejeli kwenu speaks more about maumbile yenu and not the other way around.
Vijana jifunzeni staha na kuheshimu njia mliyopita. Mgebanwa on the process msingekuwa Twitter leo kuleta haya madharau
#Tanzania
is trending in Kenya....
Sababu? Tanzania hatukipigia
#Kenya
kura kwenye baraza la usalama la UN, badala yake tuliipigia
#Djibouti
Kwa hakika, hali ya jumuia si nzuri...
I am shocked and saddened by president
@MagufuliJP
comments calling "men to direct their anger to their wives" as opposed to burning public goods. No woman should be recipient of men's anger. It's appalling for a president to promote violence against in any form or shape.
Kwa kuwa Mheshima Rais alitoa muongozo "Wote wenye kesi za uhujumu uchumi, walipe hela wanazodaiwa na wataachiwa huru"
#DPP
I am sure waTanzania tuko tayari kuchanga na tutalipa hizo 17m kabla ya jua kuzama ili
@TitoMagoti
na
@TheoGiyan
wakale xmas na familia zao
#FreeTito
Rais ajaye wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni
@TunduALissu
, ametamka leo Maalim
@SeifSharifHamad
katika Mkutano wake wa Kampeni huko
#Mahonda
, Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Niliongea na Mwenyekiti wetu wa SADC Rais
@MagufuliJP
kuhusu kuitisha mkutano wa jumuia, yeye akashauri maoni yatumwe kwa kuandika tu- Mimi bado nikaona haja ya kuitisha mkutano huu, hasa kwa nchi za kusini mwa Afrika - Rais
@CyrilRamaphosa
@PresidencyZA
Miaka 59 baada ya kupata uhuru tumesahau kwanini tulitafuta uhuru wetu. Kama issue ilikuwa madege na mabarabara, tungewaachia tu wakoloni wamalize - Dr Lwaitama
@lwaitama1
Mh Rais
@SuluhuSamia
najua mimi si mjuzi wa uongozi, ila nafikiri, ni muda muafaka upunguze mikutano (public facing events) na kukaa ofisini na timu yako kusoma mafile, kufanya uchambuzi yakinifu na kuongoza mapambano ya kuokoa maisha ya watanzania dhidi ya korona.
Mh rais wangu mpendwa
@SuluhuSamia
mimi raia wako nimekuwa nikiota sana hii ndoto ya kusameheana na kusafiana nia.
Unaonaje siku ya mwaka mpya mkanywa chai pamoja na viongozi wa upinzani wakiwemo waliomo magerezani na kufungua ukurasa mpya!
Hili liko kwenye uwezo wako Mh Rais
Rais
@SuluhuSamia
amemaliza kuongea. Hotuba ilikuwa fupi sana na kuacha mambo mengi ambayo angeyasemea. Sijui kwanini wameamuandikia a very flat speech. 😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭
Hizi ndizo jeneza "sirikali ya wanyonge/maskini" inazikia watu wake wanyonge/maskini. Wakaamua kufunika na tetron ya mita buku. Kama tumeshindwa kuwazika wanyonge (wanaosemwa ndio wenye serikali yao) kwa utu, staha na heshima, yamkini tumejua sirikali ni ya tabaka gani.
Leo niliwapeleka watoto wakajionee maajabu ya
@masoudkipanya
bahati mbaya hawakupata nafasi ya kuongea nae. Labda kaka Masoud uandae session ya kuongea na vijana wa rika hili. Ila hongera sana. Sisi pia tunaweza kuwekeza kwenye mitigation kupambana na mabadiliko ya tabia nchi.
#CAG
WON, He is our national hero and we will celebrate him
#IstandWithCAG
But do you know who else WON today? "THE CORRUPT" they will now steal without fear. Tanzanian are the main losers, very same people we mandated them to oversee the government they rejected to do so. SAD
Mimi ni Muislam, tena practising muslim ila vitu kama hivi vinanikwaza mno. Why Muslims try so hard to be in the wrong side of history? Kwani usipooa mtoto wa 9 utachoma? It's about time tuache hizi madness kwa kisingizio cha dini, no where it says, you MUST marry her at age of 9
Ila watanzania kweli hatujui kuwa tuna satellite schools? Jamani hii nchi ni kubwa mno na hizi shule ni za muhimu sana hasa kwa watoto wadogo kwenye jamii za pembezoni.
Jamani mimi naomba niulize hili swali ili nijifunze,
@yangasc1935
watapoteza nini wakimuacha Fei aende? kama kesi wameshashinda, wameshawaonyesha wachezaji wengine kuwa si rahisi kupambana na mamlaka, mechi wanashinda bila yeye nk. Kitu gani kingine Yanga wanataka kuprove?
Mbona hamjiamini?
Kama kweli nyinyi ni bora, si mje uwanjani mpimane uwezo.
Kutekana, kupigana, kunyanganyana fomu, kunasema jambo moja tu... kuwa mnajua kuwa nyinyi ni dhaifu.
Watanzania wenzangu, ukikutana na aliyekuwa mbunge, kwanza mwambie akuamkie- haijalishi kama ni mkubwa au mdogo, pili muombe hela.Tuna miezi 4 tu ya kuwaonyesha kuwa sisi ndio mabosi wao, itumeni vizuri, ila ikifika kwenye kupiga kura 2020, fanya mabadiliko ya kweli. Tuanze upya
Ni mimi tu, ninayeona kampeni ya vegetable zimepwaya? No content, no strategy... au kwao uchaguzi umeisha, wanachukulia poa? Au wakongwe wamekaa kando na ujuzi wao.
Kwa mwendo huu, upinzani wakijipanga poa, wanatoboa mchana kabisa.
Duniani kuna mashujaa halafu kuna
@TunduALissu
ambae yuko kwenye daraja la peke yake.
Sijawahi na sijui kama nitakuja kuona mtu mwenye ujasiri na ushujaa kama wake.
Kama wewe hata kutweet tu unaogopa
#TunduLissuHomeComing
ikufunze kitu.
Karibu nyumbani
So no more kelele za kodi za miamala?! Watu tuko busy na Mwenyekiti, Manara na Bata la Kigoma.
Say anything about watawala, ila tuwape heshima yao kwenye politicking! Tunapigwa matukio mpaka akili zinakaa sawa!
Hivi CCM si kuna umoja wa wanawake? Na
serikali si ina waziri wa "wanawake"? Wale wabunge wa viti maalum si bado wapo? Wanaachaje wanawake wanatukanwa na kudhalilishwa kila siku? You know what!? Tukutane 2020... Walai tutawafundisha siasa za wanawake, na mtajuta kutusaliti