Today, the World Bank has declared Tanzania Middle Income Country. In this regard, I congratulate all my compatriots for this historic achievement. We had envisaged to achieve this status by 2025 but,with strong determination, this has been possible in 2020. GOD BLESS TANZANIA.
On behalf of the Government and the people of Tanzania, I congratulate Y'r Excellency Narendra Modi on y'r re-election as Prime Minister of India.This indicates the confidence that y'r compatriots have in you. Be assured of our commitment to strengthen our bilateral co-operation
Naitwa John Pombe Joseph Magufuli, mgombea kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Ewe Mtanzania mwenzangu, naomba kura yako ya ndio tarehe 28/10/2020. Chagua Magufuli kwa maendeleo ya kweli ili tuendelee kujenga Tanzania mpya. Asante.
Benki ya Dunia leo tarehe 01 Julai, 2020 imeitangaza Tanzania kuingia UCHUMI WA KATI.Nawapongeza Watanzania wenzangu kwa mafanikio haya.Huu ni ushindi mkubwa na kazi kubwa tumeifanya, tulipanga kuingia uchumi wa kati ifikapo 2025 lakini tumefanikiwa 2020.MUNGU IBARIKI TANZANIA
Nimesikitishwa na kifo cha Mzee wetu Benjamin Mkapa (Rais Mstaafu wa Awamu ya 3). Nitamkumbuka kwa mapenzi yake makubwa kwa Taifa, ucha Mungu, uchapakazi na utendaji wake katika kujenga uchumi. Hakika Taifa limepoteza nguzo imara. Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, Amina.
Ndugu zangu Watanzania, kutokana na ugonjwa wa Corona, nawaomba tutumie siku 3 za kuanzia tarehe 17- 19 Aprili, 2020 {Ijumaa, Jumamosi na Jumapili} KUMUOMBA MWENYEZI MUNGU aliye muweza wa yote atuepushe na janga la ugonjwa huu. Tusali kwa kila mmoja kwa imani yake, atatusikia.
Nimeshtushwa na taarifa za kifo cha Rais wa Burundi, Mhe. Pierre Nkurunziza. Nitamkumbuka kwa uongozi wake imara na juhudi zake za kupigania amani, maendeleo na kuruhusu demokrasia. Kwa niaba ya Serikali na Watanzania nawapa pole familia na Warundi wote. Mungu amweke mahali pema.
Nakupongeza Ndg. Evariste Ndayishimiye kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Burundi. Wananchi wa Burundi wameonesha imani kubwa kwako. Kwa niaba ya Serikali na Watanzania wote naahidi kuendeleza uhusiano mzuri kati yetu. Nawatakia Warundi wote amani na ujenzi bora wa Taifa lenu.
NAMSHUKURU Mungu kwa kunifikisha siku ya leo.
Pia NAWASHUKURU nyote mlionitakia heri katika siku yangu ya kuzaliwa. Mmenionesha upendo wa dhati na mmenitia nguvu katika kutekeleza majukumu yangu.
Nami nawatakia afya njema, maisha marefu na Mwenyezi Mungu awabariki sana.
The Government and the people of Tanzania convey their warmest congratulations to Dr.Akinwumi Adesina on his re-election as the President of the
@AfDB_Group
. In our joint work over the last 5 years, we have appreciated your consistent commitment to Africa.
HONGERA SANA 👏🏼👏🏼👏🏼
Nawashukuru wana CCM wote na Watanzania wa vyama vyote kwa kujitokeza katika uzinduzi wa kampeni za CCM 2020 Jijini Dodoma. Pia nawashukuru wasanii, waandishi wa habari, viongozi wa Dini, n.k waliojitokeza kuniunga mkono katika uzinduzi huu. Maendeleo hayana chama. Tanzania Hoyee
Nawapongeza Walimu wenzangu wa madaraja yote kwa kuadhimisha siku ya Walimu Duniani. Serikali inatambua mchango wenu mkubwa kwa Taifa na itaendelea kuboresha maslahi na mazingira yenu ya kazi. Endeleeni kuchapa kazi. Tulianza pamoja, tutamaliza pamoja.
:
Mwl. John Pombe Magufuli.
Nakupongeza Dkt. Lazarus Chakwera kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Malawi. Kwa niaba ya Serikali na Watanzania wote naahidi kuendeleza uhusiano wetu wa kidugu, kirafiki na ujirani mwema hususani katika masuala ya uchumi na ustawi wa jamii.
Hongera sana Mhe. Rais.
On behalf of the Government and the people of Tanzania, I congratulate President-elect
@JoeBiden
and Vice President-elect
@KamalaHarris
on your victory in the US General Election. Be assured that Tanzania will continue to cherish the relationship that exist between our countries.
Nawatakia heri WAKULIMA, WAFUGAJI na WAVUVI katika sikukuu hii ya Nanenane. Serikali inatambua mchango wenu mkubwa katika ujenzi wa Taifa na ustawi wa Watanzania. Tunaahidi kuendelea kuwaunga mkono na kushughulikia changamoto zenu ili kuongeza tija katika kazi zenu. NANENANE JUU!
Nimepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha kijana wangu Ruge Mutahaba. Daima nitamkumbuka kwa mchango wake mkubwa ktk tasnia ya habari, burudani, na juhudi za kujenga fikra za maendeleo kwa vijana. Poleni wanafamilia,ndugu,jamaa na marafiki. Mungu amweke mahali pema, Amina.
Congratulations Your Excellency Mokgweetsi Masisi on your election as President of Botswana. On behalf of the Government and People of Tanzania, I wish to reiterate our commitment to further strengthen the excellent bilateral relations that exist between our two countries.
Nimesikitishwa na taarifa za kifo cha Mzee na Rafiki yangu Dkt. Reginald Mengi. Nitamkumbuka kwa mchango wake mkubwa ktk maendeleo ya Taifa letu na maono yake yaliyopo ktk kitabu chake cha I Can, I Will, I Must. Poleni wanafamilia, wafanyakazi wa IPP na Jumuiya ya Wafanyabiashara
Kwa niaba ya Serikali na Watanzania nakupa pole Mhe.Rais Uhuru Kenyatta na Wakenya wote kwa kuondokewa na Rais Mstaafu Daniel Toroitich arap Moi. Watanzania tutamkumbuka kwa uongozi wake mahiri, jitihada za kuimarisha uhusiano wetu na Kenya na kufufua Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mhe. Spika. Nakushukuru wewe na Wabunge kwa azimio la kunipongeza. Mmenitia moyo na kunipa nguvu zaidi ya kufanya kazi. Nami nawapongeza kwa kazi nzuri mnazofanya Bungeni na Majimboni kwenu. Mbarikiwe sana.Kwa niaba ya Serikali naahidi kuendelea kushirikiana na Bunge letu Tukufu.
Nawapongeza Wanawake wote kwa kuadhimisha siku hii muhimu. Mchango wenu kwa familia,jamii na Taifa hauna mfano.Serikali ninayoiongoza itaendelea kuwathamini,kuwaheshimu na kujenga mazingira bora yatakayowawezesha kutekeleza majukumu yenu ipasavyo.
#HappyInternationalWomensDay
Congratulations to Your Excellency President Xi Jinping and the people of China on commemoration of the 70th anniversary of your great Nation. On this occasion, I pledge to further enhance our historic, friendly and fraternal ties.
祝贺习近平主席!祝贺全体中国人民!
China Hoyee!
I am deeply saddened to hear about the crash of the Ethiopian Airlines' Boeing 737 which occurred early today. I seize this occasion to express my profound condolences to all the bereaved families and to all Heads of State whose people's lives have been claimed by this accident.
Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Rais Mstaafu na Baba wa Taifa la Zimbabwe Mzee Robert Mugabe. Afrika imepoteza mmoja wa viongozi Jasiri, Shupavu, Mwanamajumui wa Afrika na aliyekataa ukoloni kwa vitendo. Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, Amina.
Punde nimezungumza na Mhe. Kenyatta kuhusu shambulizi la Jijini Nairobi,zaidi ya watu 14 wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa.Pole sana Mhe. Rais na pole sana wananchi wa Kenya.Tupo nanyi katika kipindi hiki cha majonzi. Nawaombea Marehemu wote walale mahali pema peponi, Amina.
Nawapa pole familia na wote walioguswa na kifo cha Jaji Mstaafu Mark Bomani. Nitamkumbuka kwa mchango wake mkubwa Serikalini katika masuala ya sheria na katika chama akiwa Mjumbe wa Baraza la Wadhamini wa CCM. Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, Amina.
Nimesikitishwa na taarifa za kifo cha ghafla cha Rais wa Chama cha Wanamuziki wa Injili Tanzania, Dkt. Donald Kisanga aliyefariki dunia kwa ajali ya gari Jijini Dodoma. Mungu amweke mahali pema peponi, Amina.
Nawashukuru wote mlionitakia heri katika siku yangu ya kuzaliwa. Mungu ni mwema.
Nimepokea salamu nyingi japo sikuweza kuwajibu wote, lakini muamini kuwa nimezipata. Nawaomba Watanzania tuendelee kudumisha amani,upendo,mshikamano na tuchape kazi za kulijenga Taifa letu.
Hongera sana Mhe. Rais Hage Geingob. Your re-election is clear testimony of the trust and confidence that Namibians have bestowed on you. I wish to assure you of our continued support to further strengthen the historical ties between our two brotherly countries.
Following the judgement by the High Constitutional Court. I congratulate HE. Felix Tshisekedi on his election as President of the DRC. While congratulating all the Congolese, I beseech you to maintain peace and affirm my commitment to furthering our historic and brotherly ties.
Nimesikitishwa na kifo cha Mzee wetu Balozi (Mst) Job Lusinde. Nawapa pole Familia, wana Dodoma na Watanzania. Nitaukumbuka mchango wake mkubwa kwa Taifa akiwa Waziri, Balozi, Mdhamini wa CCM na Kiongozi wa Wazee wa Dodoma. Pumzika salama Mtani wangu, kazi kubwa umeifanya vizuri.
It is with deep sorrow that I received the news about the demise of the Leader of Oman Sultanate, Sultan Qaboos bin Said Al Said. During his leadership, our two nations enjoyed strong and close bilateral relations. We convey our profound condolences to all the people of Oman.
Vijana wangu - TAIFA STARS🇹🇿
Muda mfupi ujao nitakuwa nikitazama mchezo kati yenu na Timu ya Taifa ya Lesotho 🇱🇸.
Mimi na Watanzania wenzangu tunawatakia mchezo mwema, mrudi na ushindi.
Nimehuzunishwa na taarifa za kifo cha rafiki yangu Ali Mufuruki (Mwenyekiti na Mwanzilishi wa Jukwaa la Wakurugenzi Watendaji wa Kampuni - CEOrt) Nitamkumbuka kwa uzalendo na mchango wake katika kukuza sekta ya biashara na ushauri kwa Serikali.Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un.
Nawapongeza wanachama na wakereketwa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa chama chetu kutimiza miaka 43 tangu kuzaliwa. Tunaposherehekea siku hii muhimu kwa kazi tuendeleze misingi ya chama chetu, tusimamie utekelezaji wa Ilani na tudumishe amani, upendo na mshikamano.
CCM HOYEE!
Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar. Natoa pole kwa Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Mwinyi, Familia, Wazanzibari, wanachama wa ACT-Wazalendo na Watanzania wote. Mungu amweke mahali pema peponi,Amina
I'm very glad that we have commenced the second lot of our central line standard gauge railway construction from Morogoro to Dodoma. As we celebrate this important milestone in our country's development lets steadfastly preserve our peace, unity and solidality.
Nimepokea kwa mshituko mkubwa taarifa za kuuwawa askari wetu kumi na wanne na wengine arobaini na wanne kujeruhiwa na wawili hawajapatikana huko DRC wakati wakitekeleza majukumu ya ulinzi wa amani, natoa pole sana kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania na familia 1/2
I am deeply saddened by the news about the passing on of the former President of Ghana, H.E. Jerry John Rawlings. My condolences to Your Excellency Nana Akufo-Addo and the brotherly people of Ghana for the loss of this Great-man of Africa. May his soul rest in peace, Amen.
Nimesikitishwa sana na kifo cha mwanafunzi Akwilina Akwilini wa Chuo cha Usafirishaji (NIT).Natoa pole kwa familia,ndugu,wanafunzi wa NIT na wote walioguswa na msiba huu.Nimeviagiza vyombo vya dola kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua za kisheria waliosababisha tukio hili.
Cde. Mnangagwa. On behalf of the Government and people of Tanzania,I convey my sincere congratulations on your victory in the Presidential Election of Zimbabwe.Your victory is a reflection of the confidence reposed in you by the people of Zimbabwe in leading them to prosperity.
Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya ajali ya basi iliyotokea Kericho nchini Kenya na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 50. Nakupa pole Mhe. Rais Uhuru Kenyatta, familia za marehemu na Wakenya wote. Mungu aziweke roho za marehemu mahali pema na majeruhi wapone haraka.
@UKenyatta
I congratulate Your Excellency and dear brother Prof. Mutharika on your re-election as President of Malawi. On behalf of the Government and the people of Tanzania, I pledge our commitment to further strengthening our friendly and fraternal relations, in bettering our economies.
Nimesikitishwa na kifo cha Prof. Benno Ndulu (Ex-Governor BOT). Pole kwa familia na wafiwa wote. Nitamkumbuka kwa ushauri wake wa kuimarisha uchumi wa nchi yetu hususani mageuzi ktk sekta ya fedha. Alikuwa mchapakazi na mnyenyekevu. Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi,Amina
Nimesikitishwa na kifo cha Maria na Consolata. Nilipokwenda hospitali waliliombea Taifa. Walikuwa na ndoto ya kulitumikia Taifa. Poleni familia, Masista wa Maria Consolata na wote walioguswa, pumzikeni mahali pema wanangu. BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.
Nakupa pole Mhe. Rais Museveni na wananchi wote wa Uganda kwa kuwapoteza watu zaidi ya 40 katika ajali ya maporomoko ya udongo iliyotokea katika Wilayani Bududa. Watanzania tunaungana nanyi katika kipindi hiki cha majonzi na tunawaombea majeruhi wote wapone haraka
@KagutaMuseveni
Nawapongeza wanawake wote kwa kusherehekea siku yenu ya leo na hasa kwa mchango wenu mkubwa mnaoutoa kwa jamii. Daima tutaendelea kuwaheshimu, kuwapa ushirikiano na kutambua juhudi zenu katika kujenga ustawi wa jamii yetu.
Nimefurahishwa na ushindi wa Grace Products, lakini pia nimefurahishwa kwa kutumia kiswahili kukizungumza nchini Marekani, hongereni sana Grace Products.
Nakupongeza Mhe. Yoweri Kaguta Museveni kwa kutangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Uganda kuwa mshindi wa kiti cha Urais. Tanzania itaendeleza urafiki na udugu wetu kwa maslahi mapana ya wananchi. Hongereni Waganda kwa kukamilisha Uchaguzi Mkuu, endeleeni kudumisha amani na upendo.
I have learnt with deep sorrow the sad news of the demise of Winnie Mandela, a woman of an exceptional courage and strength.
She will always be remembered for the important role she played during the struggle against apartheid.
May the Almighty God rest her soul in eternal peace.
MAN OF GOD, Rev. TB JOSHUA
On behalf of my family, I extend my heartfelt wishes on your 55th Birthday. May the Almighty God bestow upon you exceeding divine inspiration so that you can bring deliverance to more people and spread his fragrance across nations. HAPPY BIRTHDAY TO YOU
Ninayo furaha kukupongeza Mzee wangu Alhaji Ali Hassan Mwinyi kwa kutimiza miaka 93. Busara zako, ushauri, upendo, unyenyekevu, ucha Mungu na ushirikiano kwa Watanzania ni jambo tunalojivunia sana. Nakutakia afya njema na maisha marefu yenye furaha na amani. HAPPY BIRTHDAY.
My heartfelt condolences to Morgan Tsvangirai’s family. Our thoughts and prayers are with the Zimbabwean people during this time of grief and inexpressible sorrow.
Nakupongeza Mhe. Rais Yoweri Museveni na wananchi wote wa Uganda kwa kuadhimisha miaka 56 ya Uhuru. Kwa niaba ya Watanzania nawaahidi kuundeleza na kuukuza uhusiano na ushirikiano wetu wa kihistoria. Kwa pamoja tudumishe ujirani mwema, udugu na urafiki kwa manufaa yetu sote.
Nawapongeza viongozi, wanachama na wapenzi wote wa CCM kwa kutimiza miaka 41. Tunaposherehekea mafanikio yetu tuendelee kutunza Amani na umoja wetu, tuchape kazi kwa maslahi ya nchi yetu na Serikali inayoongozwa na CCM.
Marehem Sokoine hatasahaulika katika historia ya Tanzania, ni wito wangu kwa watanzania tumuige na kumuishi. Ni rai yangu pia tumuenzi kwa kujenga umoja wetu , kupiga vita rushwa na kuchapa kazi . Mungu aiweke roho ya marehemu Edward Moringe Sokoine mahala pema peponi 3/3
Kwa miaka 44 chama cha CCM kimeendelea kuongoza mapambano ya kulinda heshima na uhuru wa Tanzania, kazi iliyoasisiwa na vyama vya TANU na ASP. Hongereni Watanzania; Hongereni Waafrika
Nimesikitishwa na kifo cha Kamishna wa Maadili, Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Harold Nsekela. Poleni familia, watumishi wote wa Sekretarieti ya Maadili na Mahakama. Jaji Mstaafu Nsekela alikuwa mwadilifu, mzalendo, asiyejikweza na mchapakazi. Mungu amweke mahali pema, Amina.
Katika siku kama ya leo tarehe 12 Aprili 1984 nikiwa Mpwapwa JKT nikitumikia jeshi langu “Oparesheni Nguvukazi” tukatangaziwa kifo cha marehem Edward Moringe Sokoine, ilikuwa siku ya majonzi shujaa huyu niliyemjua na kumshabikia ikawa siku yake ya mwisho 1/3
Nimesikitishwa na kifo cha Ndg. Subhash Patel. Wakati wa uhai wake ametoa mchango mkubwa katika maendeleo ya viwanda, kukuza biashara na kuzalisha ajira kwa Watanzania wengi. Natoa pole kwa Familia, CTI, TPSF na TNBC ambako alishiriki vizuri.
Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un.
Wakati tunapoazimisha siku kama hii ya kifo chake, watanzania tuige mfano wake kwani alikuwa msema kweli, asiyeogopa, mpiga vita rushwa,ufisadi, unyonyaji,mzalendo wa kweli na aliyechukia rasilimali za watanzania kuibwa 2/3