Award winning TV/Radio Personality | Hosting Amplifaya on CloudsFM |Journalist from Tanzania covering East Africa and beyond | Bookings millard
@millardayo
.com
A VERY BIG THANKS kwa yeyote aliyewahi kutumia hata kwa dakika 1 tu kwenye youtube ya millardayo, MUNGU ANA MAGUVU SANA tumefikisha VIEWS BILIONI MOJA, Youtube wametupongeza na kusema nimekua MWANDISHI/MEDIA ya kwanza AFRIKA nzima kupata 1 BILLION VIEWS!! 🙏🏿🙏🏿MAKUBWA YANAFATA !!
Hatimaye Msanii nguli wa Tanzania Joseph Haule maarufu kama Profesa Jay amerudi tena kwenye mitandao ya kijamii kwa mara ya kwanza leo ikiwa ni baada ya siku zaidi ya 462 za kutokuweka chochote kwenye kurasa zake baada ya kuugua na kulazwa Hospitali ambapo kwenye post yake leo…
Shirikisho la Soka Ulimwenguni (FIFA), limemchagua Mkurugenzi wa Sheria wa Yanga SC Simon Patrick kuwa Mwanasheria wa FIFA anayeshughulikia masuala ya migogoro ya Wachezaji Duniani kote kwa kipindi cha miaka mitatu.
#MillardAyoSPORTS
Nafahamu wengine ndio tunaianza night shift kama mimi mida hii…….. sasa nina elfu 30 tatu kwa Watu watatu ambao reply zao hapa hazitopata like hata moja!! TWENDE KAZI 😁
#BREAKING
: Aliyewahi Kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Camilius Membe amefariki dunia leo asubuhi Katika Hospitali ya Kairuki Mikocheni Jijini Dar es salaam.
Aliyekuwa Msaidizi wa Membe, Allan Kiluvya ameithibitishia
@ayotv_
kuhusu kifo cha Membe…
Uongozi wa Young Africans Sports Club umetoa taarifa kuwa umefikia makubaliano ya kuachana na Kocha wake Nasreddine Nabi baada va
Kocha huyo kuomba kutoongeza mkataba mpya.
“Mkataba wa Kocha Nasreddine Nabi na Klabu ya Young Africans Sports Club umemalizika mwisho wa msimu huu,…
Rais wa Uganda, Yoweri Kaguta Museveni amesema kama Mataifa ya Magharibi yatawanyima misaada kutokana na kupitisha sheria ya kupinga ushoga basi watakaa chini na kupunguza matumizi ya Nchi kwa kubana matumizi huku wakipanga bajeti kwa umakini lakini kamwe hawatoifuta sheria kwa…
Mchezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars Bernard Kamungo
@bernardk17
anayecheza FC Dallas ya Marekani, alfajiri ya leo alikuwa uwanjani kucheza dhidi ya Inter Miami inayochezewa na Lionel Messi katika mchezo wa Kombe la Ligi (North & Central America League Cup).
Katika…
Mwimbaji Staa wa Bongofleva Alikiba usiku wa leo ameitambulisha rasmi biashara yake mpya ya Redio kwa kuizindua Redio Stesheni yake mpya iitwayo Crown FM 92.1 ambayo inasikika Dar es salaam, Zanzibar, Tanga na Pwani.
Endelea kuwa karibu na page ya millardayo kupata info zote…
Wanafunzi 150 wa udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Tiba, Sayansi na Teknolojia (UMST) cha Khartoum nchini Sudan wamehamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ili kukamilisha mwaka wao wa mwisho wa masomo.
Akiongea wakati wa kuwakaribisha wanafunzi hao, Mkurugenzi Mtendaji wa…
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uhamisho wa baadhi ya Wakuu wa Mikoa ambapo amemuhamisha aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Albert John Chalamila kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam akichukua nafasi ya Amoss Makalla aliyehamishwa kuwa Mkuu wa Mkoa Mwanza.…
Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amemteua Paul Christian Makonda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
Kabla ya uteuzi huu Makonda alikuwa Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na anachukua nafasi ya John Vianney Mongella ambaye atapangiwa kazi…
Rais Samia ameagiza Kijana aliyewaokoa Watu 24 ajali ya ndege Bukoba atafutiwe kazi kwenye Jeshi la Uokozi “Rais ametupigia,ameagiza akabidhiwe kwa Waziri wa Mambo ya Ndani nae pia atafutiwe nafasi Jeshi la Uokozi na apate mafunzo zaidi kwa ujasiri wake".
#MillardAyoUPDATES
Club ya Pyramid FC ya Misri imetangaza kumsajili Mshambuliaji wa Kimataifa wa Congo DR Fiston Kalala Mayele (29) kutokea Yanga SC ya Tanzania.
Mayele anaondoka Yanga baada ya kucheza misimu miwili Tanzania kwa mafanikio makubwa msimu wa kwanza 2021/2022 alimaliza nafasi ya pili…
Mtangazaji Mkongwe wa CloudsFM Gardner G. Habash amefariki dunia asubuhi ya leo katika Hospitali ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) alikokua amelazwa kwa siku kadhaa akipatiwa matibabu.
#RIPCaptain
🙏🏿🙏🏿
Burkina Faso na Mali kwa pamoja zimewaonya Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Kiuchumi ya Afrika Magharibi (ECOWAS) kwamba wakithubutu kuvamia Nchi ya Niger ili kuwakabili Wanajeshi waliompindua Rais wa Nchi hiyo basi itakuwa ni sawa na kutangaza vita na Nchi hizo pia na hawatosita…
Club ya Simba imetangaza rasmi kumrejesha Luis Jose Miquissone (Konde Boy) Raia wa Msumbiji katika kikosi chao kwa Mkataba wa miaka miwili.
Miquissone amejiunga Simba SC kama Mchezaji huru baada ya kuondoka Simba SC 2021 na kujiunga na Al Ahly ya Misri kwa Mkataba wa miaka minne…
Ni wiki nyingine tena ya kushinda mtonyo kutoka kwa BLUE BOY WA KISHUA…. nina elfu thelathinithelathini zenye ujazo wa lunch box kwa Raia watano ambao comments zao hapa hazitopata like hata moja……. TWENDE KAZI
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amekaidi wito wa Mataifa ya magharibi wanaotaka sheria kali dhidi ya ushoga ifutwe ikiwa ni moja ya sheria kali zaidi duniani ambapo Mtu yeyote anayesambaza ushoga anaweza kuhukumiwa kwa kifungo cha kifo ambapo amesema sheria imeshapita na haiwezi…
Boss wa Makampuni ya SpaceX, Tesla na Twitter, Elon Musk(52) ametangaza kubadilisha logo ya Twitter kutoka logo ya ndege na sasa inakwenda kuwa alama X ambayo itaanza kutumika leo Jumatatu akisema X inamaanisha Twitter sasa unakuwa ni Mtandao wa kila kitu.
Elon amesema Twitter…
Rais wa heshima wa Club ya Simba Mfanyabiashara Mohammed Dewji amesema anakaribia kukata tamaa kutokana na mchakato wa mabadiliko wa Club hiyo kutokukamilika hadi sasa huu ukiwa ni mwaka wa sita.
Mo ameandika hayo kwenye ukurasa wake wa twitter ———> “Transformation ya Simba bado…
Msanii wa Hiphop Nay wa Mitego amesema amepokea barua ya wito kutoka Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) ikimtaka kufika Ofisi za BASATA leo saa nne asubuhi kuhusu wimbo wake mpya wa Amkeni lakini ameshindwa kufika kwakuwa yupo safarini “Mwanasheria wangu ameshafanya mawasiliano…
#BREAKING
: Aliyekuwa Naibu Waziri wa Afya Faustine Ndugulile
@DocFaustine
ameibuka mshindi wa kura za maoni Kigamboni kwa kupata kura 190, mshindi wa pili ni aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa DSM Paul Makonda mwenye kura 122.
#MillardAyoUPDATES
Baada ya juhudi za Mchezaji Feisal Salum “Fei Toto” kugonga mwamba mara mbili TFF kwa kushindwa kukubaliwa ombi lake la kuvunja mkataba na Yanga, Mchezaji huyu leo ametangaza kuomba msaada wa pesa kwa Watanzania ili aweze kwenda kwenye Mahakama ya usuluhishi wa kimichezo (CAS).…
“Asante Mungu katikati ya machozi umenipa zawadi, mimi niliyeitwa tasa ulinipa Mtoto Keagan ambaye alishangaza ulimwengu kwa ujio wake, ukaona haitoshi leo umenipa DOUBLE PORTION, leo umenipa Mapacha tena Wakiume na Wakike, hii yote ni kutangaza UKuu wako maishani mwangu”-MAKONDA
“Baba wa Taifa Mwl.Nyerere mlimpa miaka 27, akaja Mwinyi mkampa miaka 10, akaja Mzee Mkapa (Mungu amlaze mahali pema) mkampa miaka 10, amekuja Kikwete mkampa miaka 10, Mimi nina dhambi gani mnataka mnipe miaka 5 tu!?, nawaomba nipeni miaka mingine 5 zaidi”-JPM
#MillardAyoUPDATES
#BREAKING
: Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Edward Lowassa (70) amefariki Dunia leo February 10,2024 katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais , Dkt. Philip Mpango ametangaza taarifa za kifo cha Lowassa muda huu akiwa LIVE kupitia TBC.…
Mtangazaji mahiri Salim Kikeke ambaye mwezi April 2023 alitangaza rasmi kuacha kazi kwenye Shirika la Utangazaji la BBC, ameamua kurejea nyumbani Nchini Tanzania baada ya kuishi Uingereza kwa miaka 20.
Kwenye mahojiano mafupi na Millard Ayo,
@Salym
baada ya kuulizwa kama anarudi…
“Shule nyingi ni za kutwa chache za bweni lakini zina wanafunzi wengi, ni hatari kuruhusu wanafunzi warudi shule/vyuoni, acha watoto waendelee kula bata nyumbani wakati tunapambana na corona, hata wakikosa muhula wote au mwaka mzima ni bora kuliko kukoa uhai wao” -MUSEVENI
Club ya Singida Big Stars leo imetangaza rasmi kuuzwa na sasa itakuwa inamilikiwa na Japhet Makau.
Singida baada ya kuuzwa imebadilishwa jina na sasa itakuwa ikijulikana kama Singida Fountain Gate FC.
Japhet Makau ni mmiliki wa shule za Fountain Gate pia ndio mmiliki wa timu za…
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA ) Freeman Mbowe amewaongoza Viongozi, Wafuasi na Wananchi mbalimbali katika maandamano ya amani katika Jiji la Arusha leo ambayo yanatarajiwa kuhitimishwa kwa mkutano wa hadhara katika uwanja wa relini, hii ni moja ya…
Club ya PSG ya Ufaransa imekubali dau la Al Hilal lililoweka rekodi ya dunia la pound milioni 259 kumnunua Kylian Mbappe na sasa Mabingwa hao wa Ufaransa wametoa ruhusa kwa Wasaudia hao kufanya mazungumzo na Mbappe.
Paris Saint-Germain wanaamini kuwa angalau vilabu vitano vina…
Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, ametia saini moja ya sheria kali zaidi duniani dhidi ya Watu wanaojihusisha na vitendo vya ushoga, Spika wa Bunge Anita Among ametangaza mapema hii leo na kupuuzia vitisho na hatari za vikwazo kutoka kwa Wafadhili kutokea Nchi za Magharibi.…
Club ya Simba imemtangaza rasmi Mwimbaji staa wa Bongofleva Alikiba kuhamia kwenye Club hiyo na kuthibitisha kuwa atakuwa Mtumbuizaji mkuu August 6 2023 siku ya Simba day itayofanyika kwenye Uwanja wa Mkapa Jijini Dar es salaam.
Simba imeandika yafuatayo kwenye ukurasa wake wa…
Club ya Yanga imetangaza rasmi kuwa imemsajili aliyekuwa mchezaji Mwandamizi wa Simba SC Jonas Gerald Mkude kama Mchezaji huru baada ya Mkataba wake na Simba SC kumalizika.
Huu unakuwa ni usajili wa tatu wa Yanga msimu huu baada ya kumsajili Kibabage na Gift Fred kutoka SC Villa…
Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba SC Ahmed Ally kupitia Simba TV ametangaza kuwa Simba SC imeistaafisha jezi namba 20 iliyokuwa inatumiwa na Kiungo wao Jonas Mkude hadi pale atakapopatikana Mtu sahihi kutokea Simba B atakayeirithi ambapo Mkude ameondoka Simba SC…
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Dkt. Eliezer Feleshi amewasilisha muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali wa mwaka 2023 Bungeni Jijini Dodoma ikiwemo Sheria ya Mazishi ya Viongozi wa Kitaifa, Sura ya 419 ambapo pamoja na mambo mengine marekebisho haya yanakusudia…
Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir leo katika swala ya Eid katika Msikiti wa Mfalme Mohamed VI Kinondoni amewaomba Viongozi wa Serikali na Wadau kusaidia upatikanaji wa darubini ya kukusanya taarifa za mwandamo wa mwezi ili kumarisha uhakika wa taarifa.
#MillardAyoUPDATES
Shirikisho la Soka Ulimwenguni FIFA leo limetaja timu ambazo zipo katika nafasi ya kuweza kuwania kucheza fainali za kombe la Dunia kwa vilabu 2025.
Tanzania na Afrika Mashariki ni Simba SC pekee ndio imekidhi vigezo vya kuwa katika timu 12 zenye nafasi ya kupambana kwenye…
Bondia Hassan Mwakinyo (
@JrMwakinyo
) ameshinda pambano usiku huu kwa kumpiga Bondia wa Ghana Elvis kwa KO katika round ya 7 ya pambano hilo la kuwania ubingwa wa WBO Africa ambalo limepigwa New Amaan Complex Zanzibar.
#MillardAyoSPORTS
#BREAKING
FIFA imeiagiza Wydad Casablanca ya Morocco kumlipa Mchezaji Mtanzania Simon Msuva zaidi ya dola za kimarekani laki 7 ( Tsh. zaidi ya bilioni 1.6) baada ya Mchezaji huyo kushinda kesi ya madai aliyoifungua akiidai mishahara na ada ya usajili.
#MillardAyoBREAKING
Rais wa Marekani, Joe Biden ameilaani sheria mpya iliyotiwa saini na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni dhidi ya vitendo vya ushoga na kusema kuwa Marekani inaweza kuiwekea Uganda vikwazo huku akitoa wito wa sheria hiyo kufutwa mara moja.
Sheria hiyo mpya itawalazimu Watu…
Mchezaji Paul Pogba ambae ni Muumini wa dini ya Kiislamu amejitoa katika kikosi cha Timu ya Taifa ya Ufaransa baada ya kuchukizwa na kauli ya Rais Macron wa Ufaransa kusema “dini ya kiislamu ndio chanzo cha ugaidi wa kimataifa”
#MillardAyoSPORTS
Mbunge wa Tarime Vijijini, Mwita Waitara ametoka nje ya ukumbi wa Bunge huku akivua koti na tai yake baada ya kuonesha kutoridhidhishwa na majibu ya Serikali Bungeni wakati wa kipindi cha maswali na majibu Jijini Dodoma leo May 9, 2023.
Mbunge Waitara alitaka kujua lini Wananchi…
Aliyewahi kuwa Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika (PAP) na Mbunge wa Shinyanga Mjini, Stephen Masele amesema Yanga inaweza kukata rufaa CAF kupitia kifungu cha sheria za mpira za CAF namba XVI kifungu namba 3 kupinga kitendo cha kukataliwa goli alilofunga Aziz Ki.
Masele…
Club ya Al Ahly ya Misri imevunja mkataba na Mchezaji wa Kimataifa wa Msumbiji Luis Jose Miquissone kwa makubaliano ya pande zote mbili, taarifa iliyotolewa na Wakala wa Mchezaji huyo imethibitisha.
Miquissone alijiunga na Al Ahly ya Misri akitokea Simba SC ya Tanzania 2021 ila…
Ni vibe la hela yote, ni shangwe za volume yote, ni cheers za glasi zote kwa Mashabiki, Wafuasi na Wa-Cloudsnia wote ndani na nje ya Tanzania leo baada ya Mfalme wa show za mchana Mtangazaji Hamisi Mandi maarufu kama B Dozen, B12, B Twangala kutangaza kurejea rasmi Clouds Media…
Mshambuliaji wa Kimataifa wa Senegal Sadio Mane (31) amejiunga na Club ya Al Nassr ya Saudi Arabia kwa mkataba wa miaka mitatu akitokea FC Bayern Munich ya Ujerumani.
Mane anayeenda kucheza timu moja na Cristiano Ronaldo atakuwa akilipwa mshahara wa pound 650,000/= (Tsh Bilioni…
UPDATES: Qailah Nurdin Bilal ambaye ni Mtoto wa Msanii wa Bongofleva Shetta, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Chipukizi Taifa katika Chama cha Mapinduzi (CCM) katika mkutano wa 9 wa Chipukizi Taifa uliofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma.
Qayllah ameshinda kwa…
TAKUKURU Ilala imemuonya Hashim Rungwe, mgombea Urais (CHAUMMA) kuwa kugawa chakula (ubwabwa) kwenye kampeni ni rushwa na ni kosa kisheria, Rungwe amesema atatumia ubwabwa kama Vyama vingine wanavyotumia Wasanii na amewataka wajiandae kupelekana Mahakamani.
#MillardAyoUPDATES
Klabu ya Yanga SC ikiwa imepita siku moja tangu itolewe katika michuano ya CAF Champions League hatua ya robo fainali katika mchezo dhidi ya Mamelod Sundowns imeandika barua ya malalamiko kwa CAF kufuatia kukataliwa kwa goli la Azizi Ki dakika ya 58 pasipo Refa wa mchezo huo Raia…
Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) iliyokutana leo April 03, 2024 Jijini Dar es salaam, katika kikao chake maalum, chini ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na masuala mengine imemchagua Jokate Urban Mwegelo kuwa Katibu Mkuu wa…
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma CGF (Mst.) Thobias Andengenye amekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni zikionesha Watu ambao wanatajwa kuwa ni Wafanyakazi wa ajira mpya za Serikali wakiwa wamechafuka baada ya kuwasili Mkoani humo kuanza kazi katika vituo walivyopangiwa.
Andengenye…
Mchekeshaji na Mwigizaji Legend wa Nollywood Nigeria John Okafor maarufu Mr Ibu, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 62, Vyombo mbalimbali vya Habari Nchini Nigeria vimeripoti.
Ripoti zinasema Mr. Ibu amefariki akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali Jijini Lagos March…
#UNAAMBIWA
Mwanahisabati, Mwanafizikia na Mwanateknolojia wa Uingereza Isaac Newton aliwahi kuwa ‘Mbunge’ kwa mwaka mmoja tu na alikua mkimya sana, wanasema aliwahi kuongea sentensi moja tu Bungeni na sentensi yenyewe ni kumuomba mwenzake afunge dirisha. 😀🤔
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amesema kuna mkakati unaoratibiwa na makundi matano kuangamiza maisha yake, ameandika haya kwenye Instagram yake.
#MillardAyoUPDATES