Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira amefariki dunia leo wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mount Meru, Arusha, ndugu wa familia wamethibitisha
Mbunge wa Kawe Halima Mdee amesimamisha shughuli za Bunge kwa dakika moja baada ya kuingia bungeni, lakini Spika Job Ndugai akaonya kuwa shangwe za wenzake zinaweza kumponza
#MwananchiUpdates
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Tedros Ghebreyesus amesema idadi ya wagonjwa wa virusi vya corona inayoripotiwa barani Afrika huenda sio sahihi kwa kuwa vipimo sio thabiti
#MwananchiUpdates
“Kumpenda Mungu huku tukiwatesa na kuwadharau wanadamu ni ibada ya sanamu na Mungu hawezi kuwa upande wetu hata kama tunamuimba kila siku na kula viapo kwa jina lake.” Dk Bagonza
#MwananchiUpdates
"Kuanzia leo Machi 8, 2020 mwanaume yeyote atakayempiga mke wake nitakula naye sahani moja, chukueni namba yangu 0682009009 pigeni simu halafu kazi niachieni mimi" Paul Makonda, RC Dar es Salaam
#MwananchiUpdates
Aliyekuwa katibu mkuu wa Chadema, Dk Vicent Mashinji alivyoingia mahakamani Kisutu leo, Mbunge Halima Mdee akataa kumsalimia.
Mashinji na viongozi 8Chadema wanakabiliwa na mashtaka 13 yakiwamo ya kula njama, kufanya mikusanyiko na maandamano yasiyo halali na ya uchochezi wa uasi.
"Maisha ni magumu fedha hakuna watu wana hali mbaya akina mama wananyang’anywa televisheni, friji kwa ajili ya mikopo. Tunaomba mheshimiwa tuachie fedha mengine yote hatuna tatizo na wewe,” amesema Abel Mpinga, mkazi wa Wilaya ya Igunga mbele ya Rais John Magufuli
Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (Chauma), Hashim Rungwe amesema chama hicho hakitashiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika Novemba 24, 2019.
#MwananchiUpdates
Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa amemteua aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu Tanzania, Profesa Benno Ndulu kuwa mmoja kati ya watu 18 wanaounda baraza la kumshauri katika uchumi
#MwananchiUpdates
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ameomba msamaha kwa Wakenya kufuatia kitendo cha polisi kutumia nguvu kuwatawanya wananchi waliokutwa nje baada ya katazo la kutotoka nje kuanzia saa 1 usiku hadi saa 11 alfajiri kuepuka maambukizi ya corona
#MwananchiUpdates
“Tanzania ilikuwepo kabla ya Mheshimiwa Magufuli (Rais) na itakuwepo baada yake. Tanzania si mali ya mtu awaye yeyote bali ni mali ya Mungu muumbaji wa mbingu na nchi.” - Askofu Stephen Munga. Soma zaidi >
Mama mzazi wa mwandishi Erick Kabendera, Verdiana Mjwahuzi amefariki dunia leo Jumanne Desemba 31, 2019. Mtu wa karibu na familia amethibitisha
#MwananchiUpdates
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kuanzia kesho Jumatatu Aprili 6 watu wanaozurura bila kazi watakamatwa ili kuepusha maambukizi ya virusi vya corona
#MwananchiUpdates
Spika Job Ndugai amesema wanamsubiri Mbunge Zitto Kabwe awaeleze kwanini aliandika barua kwa benki ya dunia kuzuia mkopo kwa ajili ya elimu nchini
#MwananchiUpdates
“Niliwahoji wanaogopa nini wakati wana uwezo wa kukata jina langu? Niliwaambia waniache nigombee halafu huko mbele wakate jina langu maana si uwezo wanao bwana,” - Bernard Membe. Soma zaidi hapa>
"Tanzania ipo uchumi wa kati lakini mimi siwezi kumudu familia yangu kunywa chai ya maziwa ingawa baba yangu pale Tanga tulimudu kunywa chai ya maziwa enzi hizo.
Uchumi lazima uendane na maisha ya wananchi kuwa na mabadiliko hata ya kimaisha," amesema Profess Mussa Assad
CAG Profesa Mussa amesema mashirika ya umma 14 ikiwemo Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) na Benki ya TWB yana matatizo ya kifedha na kusababisha kuwa na madeni makubwa kuliko mtaji wake, kati ya mashirika hayo, 11 yana ukwasi hasi na mengine kujiendesha kihasara kwa miaka miwili.
NUKUU: "Hauwezi kubadilisha dunia. Hiyo ni kazi kubwa. Mpigie mzazi wako simu, mwambie umemkumbuka na unampenda. Mtakie maisha marefu. Gusa maisha ya mtu mmoja mwenye uhitaji, leo na kesho na keshokutwa. Kwa kufanya hivyo, dunia itabadilika yenyewe"-
@KennedyMmari
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo ya faragha na Mwanasiasa Mkongwe ambaye ni Mwanachama wa Chama cha ACT Wazalendo Maalim Seif Sharif Hamad, Ikulu Jijini Dar es Salaam.
#MwananchiUpdates
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa ofisi ya chama hicho kata ya Ndala manispaa ya Shinyanga huku akiwataka wanachama wa chama hicho kufanya kazi kwa kushirikiana.
#MwananchiUpdates
“Ninakusudia kuunda kamati ya wataalamu waliangalie suala la corona kwa upana halafu watushauri serikali, watupe upeo wa tatizo hili lilivyo na hayo yanayopendekezwa na ulimwengu, hatuwezi kujitenga kama kisiwa na hatuwezi kupokea yanayoletwa bila kufanya utafiti,” –
@SuluhuSamia
Baada ya Rais wa Tanzania John Magufuli kufariki dunia, hakuna uchaguzi mwingine unaofanyika badala yake, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan ataapishwa kuwa Rais kwa kipindi kilichosalia katika muhula wa miaka mitano.
"Nashukuru Mhe. Ndugai uko hapa. Kazi ya Bunge ni kutetea maslahi ya wananchi. Teteeni maslahi ya wananchi mnaowawakilisha, kama kweli tunasema tumejifunza kutoka kwa Dk Mengi."- Askofu Mkuu wa KKKT, Dk Fredrick Shoo.
#mwananchiupdates
Waumini wakiwa kwenye Ibada ya Sikukuu ya Pasaka iliyofanyika katika Kanisa la kinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT) Usharika wa Kanisa Kuu la Mjijini Dodoma leo. Picha na Anthony Siame
#MwananchiUpdates
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali haitamvumilia yeyote atakayemkwaza mwandishi wa habari akiwa kazini kwani hiyo sio sera ya Serikali.
#MwananchiUpdates
Tundu Lissu ameshinda pingamizi la Serikali dhidi ya maombi yake ya kibali cha kufungua kesi kupinga kukoma kwa ubunge wake, Mahakama Kuu imekubali kusikiliza maombi yake
#MwananchiUpdates
Rais Magufuli amesema Serikali imeamua kutowazuia watu ndani ya nyumba zao wala kufunga mipaka kwa sababu ya ugonjwa wa corona kwakutambua madhara yanayoweza kujitokeza kwa kufanya hivyo ndani ya nchi na kwa nchi 8 zinazotegemea huduma na bidhaa kupitia Tanzania
#MwananchiDigital
Rais wa Tanzania, John Magufuli amesema inawezekana Ikulu ya Dodoma ikawa ya kwanza kwa ukubwa duniani kwa kuwa ina ukubwa wa kilometa za mraba 34.5.
#MwananchiUpdates
"Juzi nilikuwa namskia Mh Jafo, mtu mmoja kule Kilosa nafikiri alichana kitabu kitakatifu, nakushukuru umechukua hatua ya kumsimamisha kazi, lakini mimi namfukuza moja kwa moja muandikie barua ya kuondoka, ashinde kesi asishinde huyo si mfanyakazi wa serikali" - Rais
@MagufuliJP
Mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi mkoani Mwanza, Jessy Mikofu amekamatwa na polisi kwa amri ya mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Philis Nyimbi kwa madai ya kupiga picha watu waliokuwa wakidai huduma ya kupata vitambulisho vya Taifa katika ofisi za Mamlaka ya Vitambulisho vya
Serikali imekiri kupokea barua ya mwanaharakati wa haki za binadamu nchini, Tito Magoti aliyemwandikia Rais Samia Suluhu Hassan, akilalamikia mfumo wa sheria unaokandamiza haki za watuhumiwa na kusababisha kukaa mahabusu kwa muda mrefu
Rais John Magufuli amemlipia Sh38 milioni Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa kati ya Sh40 milioni alizotakiwa kulipa faini baada ya kuhukumiwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
#MwananchiUpdates
“Hatutasahahu kitendo cha Rais Kenyatta cha kutukumbusha umuhimu wa kuheshimu dini na Imani za wengine kwani alisitisha kuhutubua akiwa jukwaani ili kupisha adhana iliyokuwa inasomwa msikitini imalizike na ndipo alipoendelea, alituachia gumzo na funzo kubwa sana,” -
@SuluhuSamia
Aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad amesema watu wenye tabia ya kuunga mkono kila wakati ni wasaka fursa na hawana msaada wowote katika nchi.
Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Dk Edward Hoseah amesema si kosa kwa wananchi kudai Katiba Mpya na kwamba wakati umefika kwa mamlaka za nchi kutoa mwongozo mpya wa kufikia hatima ya dai hilo.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee ametoa maelekezo kwa wakuu wa Magereza nchini kuanza kujitegemea kwa chakula cha wafungwa pamoja na huduma nyingine kuanzia Machi 1, 2020
#MwananchiUpdates