Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam, imetengua uamuzi wa kamati ya maadili ya mawakili, ambayo ilimfuta uwakili, Fatma Karume na kuagiza uamauzi huo uliotokana na malalamiko yaliyotolewa na mwanasheria mkuu yapelekwe kwenye kamati hiyo na Fatma apate nafasi ya kujitetea.
Mtangazaji maarufu wa BBC, Zuhura Yunus ametangaza kuondoka ndani ya shirika hilo alilolitumika kwa miaka 14 kwa mafanikio makubwa. Zuhura raia wa Tanzania, alijiunga na BBC mwaka 2008 atatangaza kipindi cha mwisho leo Ijumaa saa 3:00 usiku cha Dira ya Dunia.
HABARI: Wagombea udiwani na ubunge, kusanyeni matokeo yenu ya uchaguzi, fanyeni mahesabu, kama mtakuta mnaongoza iambieni dunia kuwa naongoza, si kosa kisheria kusema mimi ninaongoza, halafu ndiyo muende kwa mkurugenzi na fomu zenu mumuambie tangazeni matokeo – Tundu Lissu
Kuna hii kitu ya kusema Rais amefanya hiki na kile, tujenge utaratibu wa kusema serikali imefanya hivi. Lazima tuwe kama timu, wote tushughulike tusijenge utaratibu wa kuwafanya wananchi waamini ni mtu mmoja tu ndiyo anaweza kufanya- Jaji Joseph Warioba
Nimekuwa msomaji mzuri wa makala za Jenerali Ulimwengu na amekuwa kama hazina, kama kuna jambo la kusema atalisema, kuna watu wamekuwa mazuzu, mtu amesoma, anamwogopa mtu kwa sababu anatumia V8, nyumba ya serikali, anagopa nikitoka hapa nitapata riziki wapi, si sawa- Prof. Mussa
Mahakama Kuu, imebatilisha hukumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ya kesi ya Jinai iliyokuwa ikimkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake 7 na kuamuru warejeshewe fedha walizolipa kama faini, kiasi cha Sh.350 milioni. Uamuzi huo umetolewa leo na Jaji Irvin Mgeta.
WAZIRI Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Sinde Warioba, ameeleza kuwa Balozi Bashiru Ally, hajafanya kosa lolote hakustahili kushambuliwa. Amesema, watu wajibu hoja badala ya kumshambulia yeye binafsi.
Mbunge wa Kawe, Askofu Josephat Gwajima amesema tumerudi uchumi wa chini kwasababu, "kilichotuingiza uchumi wa kati tumekiacha ndiyo maana tumerudi tulipokuwa, hii ndiyo maana ya kukosa dira ya Taifa na maoni ya Taifa."
HABARI MPYA: Tundu Lissu, aliyekuwa mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema, ameondoka nchini humo leo Jumanne kwenda Ubelgiji huku akisema “sikimbii mapambano, ila nakwenda uwanja mwingine mpya wa kudai haki, demokrasia na utu wetu kwa nchi yetu.”
#MwanaHALISIDigital
Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maaendeleo (Chadema), amesema ataandika barua ya kuomba ridhaa ya chama chake kugombea kiti cha urais kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020.
#MwanaHALISIDigital
SIASA: Mgombea urais kupitia Chadema, Tundu Lissu amesema, mshindani wake, Rais John Magufuli wa CCM hakuwa amejiandaa na kinyang’anyiro hicho “ndio maana mnaona shida anazopata, alikuwa amejiandaa kutawazwa rais, hawakuwa wametegemea uchaguzi wa aina hii."
#MwanaHALISIDigital
Taarifa zilizotufikia hivi punde Jeshi la Polisi Dar es Salaam limemkamata Ofisa wa TRC aliyefukuzwa kwa kukosoa tozo, Jonas Afumwisye akiwa nyumbani kwake. Wakili wake Peter Kibatala amesema Afumwisye amempigia simu na kumweleza kuwa Polisi wamemfuata na kuelekea Central Polisi
Baada ya aliyekuwa RC wa Dar, Paul Makonda, leo Alhamisi kutotokea mahakamani katika kesi aliyofunguliwa na Saed Kubenea, kwenye Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni, Wakili Hekima Mwasipu amedai wanampango wa kuiomba mahakama itoe wito mpya baada ya juhudi za kumpata kushindikana.
PICHA: Godbless Lema, mgombea ubunge Arusha Mjini kupitia Chadema, amezindua kampeni za kutetea jimbo hilo katika mkutano uliofanyika Soko Kuu la Arusha.
#MwanaHALISIDigital
HABARI MPYA: Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wanne, leo Ijumaa, wako mahabusu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, wakisubiri kupandishwa kizimbani wakati wowote kuanzia sasa.
Mbunge wa Buchosa, Eric Shigongo (CCM) leo Jumamosi amesema Rais Samia Suluhu Hassan tangu aingia madarakani tarehe 19 Machi, 2021 ametumia muda wa saa 263 angani kusafiri kuelekea nchi mbalimbali kuwatafutia Watanzania riziki.
TAARIFA: Leo Ijumaa
@TunduALissu
mgombea urais wa Tanzania kupitia
@ChademaTz
anamaliza kutumikia adhabu ya siku saba kutofanya kampeni iliyotolewa na Kamati ya Maadili ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). Kesho atakuwa mikoa ya Dodoma na Singida
#MwanaHALISIDigital
Kwenye miaka hii mitano, tutaendelea kuimarisha misingi ya utoaji haki, usawa, uhuru na demokrasia nchini na kukuza mahusiano ya kimataifa. Nadhani mmeanza kuona hatua tulizochukua-Rais Samia Suluhu Hassan.
TAARIFA: Alicia Magabe, mke wa mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema, Tundu Lissu kesho Jumapili atakuwa mgeni rasmi katika kongamano la wanawake Arusha Mjini.
#MwanaHALISIDigital
“Siwezi kuwasema wenzangu (wanaotaka kugombea urais CCM) sababu watafukuzwa chama, nakuapia leo kama tusingekuwa tunafukuzana, ningekupa majina yote sita mimi ni wa saba, lakini watafukuzwa kesho asubuhi.” Bernard Membe.
#MwanaHALISIDigital
MSAKO: Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Dar es Salaam, Ramadhani Kingai amesema, wanamsaka mwanaharakati anayejiita Kigogo katika mtandao wa Twitter, kwa tuhuma za kuzusha hofu na uongo kwamba Rais John Magufuli anaumwa.
ZITTO: NITAMPIGIA KURA LISSU
Kwa nafasi ya Rais wa Tanzania, Mimi Zitto Kabwe, nitapiga kura Tundu Lissu. Huyu ndiye mgombea wa upinzani ambaye ana nguvu ya kumshinda mgombea wa chama tawala, amefanya kampeni nchi nzima, mwitikio wa wananchi kwake ni mkubwa - Zitto Kabwe
Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amesema, kwa takwimu zilizopo deni la taifa limefikia Sh.64 trilioni. Awamu ya tatu zilikopa dola bilioni 9, awamu ya nne dola bilioni 7 kwa miaka 10, awamu ya tano kwa miaka 5 zimekopwa dola bilioni 9. Naomba ufanyike ukaguzi ili tujue kilikopwa nini
LISSU ATIKISA CHATO
Tundu Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema, amepata mapokezi makubwa kwenye mkutano wake wa kampeni Jimbo la Chato mkoani Geita jana jioni Jumanne.
SIASA: Wanaofikiria mgombea huyu atatishwa na tume, hawanijui na niwatoe wasiwasi watu wangu, hakuna habari ya kwenda Dodoma kesho na kama itakuwepo wafuate maadili waliyoyatunga wao wenyewe ikiwemo kunipa saa 48 kuwasilisha utetezi wa tuhuma ninazokabiliwa nazo - Tundu Lissu
Vijana wangu, tumieni mitandao vizuri, kama una jambo la kulaumu, laumu na toa ushauri , kama unakosoa kosoa na toa mapendekezo nini kifanyike-Samia Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania
Sitaki kumjibu Polepole, kwenye CCM ni mchanga, ni sawa sawa na mtoto wa darasa la kwanza anajibiwa na wa chuo kikuu. Polepole ni sawa na unyasi mkavu. Siku Polepole anaingia kwenye chama kujitangaza, alipewa nguo za CCM na Nape Nnauye- Abdallah Bulembo
Mahakama Kuu ya Tanzania, leo Alhamisi, imemuamuru Mmiliki wa Gazeti la Tanzanite, Cyprian Musiba kumlipa Sh.6 bilioni, waziri wa zamani wa Mambo ya Nje, Bernard Membe kama fidia ya kumchafua kupitia vyombo vyake vya habari.Hukumu hiyo imetolewa na Jaji Joacquine De Mello.
Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP), Sylvester Mwakitalu, amewafutia mashtaka watuhumiwa 18 kati ya 36 ya ugaidi yaliyokuwa yakiwakabili viongozi wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) .
SIASA: Zimebaki siku kumi tu, katika siku hizi kumi, hakikisheni mnahamasishana kila mmoja wenu, uwe CCM umepigwa, uwe Chadema umepigwa, uwe huna chama umepigwa. Sababu tumepigwa wote, tuhamasishane tarehe 28 Oktoba wote tukapige kura- Tundu Lissu, mgombea urais wa Chadema
SIASA: Nataka kufunga bao dakika ya 89 kutoka benchi. Watanzania mkae macho na mkae chonjo. Tumefanya kazi huku chini sasa tunakuja juu kupata bao la ushindi dakika 89 na dakika za nyongeza- Bernard Membe, mgombea urais, ACT-Wazalendo
#MwanaHALISIDigital
TAARIFA: Bernard Kamilius Membe, mgombea urais wa Tanzania kupitia ACT-Wazalendo, leo Jumatatu saa 4:30 asubuhi atazungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
#MwanaHALISIDigital
Mgombea wa upinzani nchini Malawi, Lazarus Chakwera anaongoza kwa asilimia 61.3 ya kura zilizohesabiwa katika uchaguzi wa marudio nchini humo, Rais Peter Mutharika anafuatia akiwa na asilimia 38.01. Ujumulishaji wa matokeo unaendelea.
#MwanaHALISIDigital
HABARI: Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania, Bob Wangwe amesema, Asasi za kiraia, zimeomba kukutana na Rais Samia Suluhu Hassan, kwa ajili ya kujadiliana nae masuala mbalimbali ikiwemo ufufuaji wa mchakato wa katiba mpya na ushirikiano baina ya asasi hizo na serikali.
“Vita hii ya ugaidi ni ngumu, inahitaji umakini mkubwa kwa sababu mbinu wanazotumia katika mapigano hayo sio ule utamaduni wa mapigano ya kawaida, wanapigana katika vikundi vidogo vidogo,” Jenerali Venance Mabeyo.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba amefanya uteuzi wa watu mbalimbali watakaotoa elimu ya mlipa kodi kwa Watanzania wakiwemo;
@Samagoal_77
@EdoKumwembe_
na Hamisa Mabeto.
SIASA: Leo sina mengi ya kuzungumza, ila nawashukuru wote kwa hali na mali kwa support yenu kipindi ambacho mme wangu kipenzi alipokuwa anaumwa ambaye sasa hivi anaweza kusimama na kugombea nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungamno wa Tanzania – Alice Magabe, mke wa Tundu Lissu
Muda wa mafunzo ya ualimu katika vyuo vikuu uongezwe, uwe miaka minne na ule mwaka wa nne wote watumike kwenye mafunzo shuleni. Kwa hiyo tutapata walimu kati ya 15,000 mpaka 20,000 kila mwaka kutoka vyuo vikuu na hawa hatuwalipi –Mbunge wa Ubungo, Prof. Kitila Mkumbo.
Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Profesa Edward Hoseah amesema, Halima Mdee na wenzake 18 "hawapaswi kuendelea kufanya kazi za kibunge mpaka suala la uanachama wao litakapopatiwa ufumbuzi."
"Mimi wala sio Mwanachama wa Simba mimi ni Mwanachama wa Coastal Union, na ile picha ni ya zamani, nilitumwa niende kwenye Simba Day kumuwakilisha kiongozi wangu wa kipindi hiko, nilivyofika pale nikapewa ile jezi nivae, lakini nilienda na nguo tofauti" Wallace Karia, Rais wa TFF
Sikilizeni, huu moto ni kuanzia sasa hadi Ikulu na kuanzia leo wakati tunasubiri Mwenyekiti (Freeman Mbowe) azungumze. Tumewapiga mahakamani, tutawapiga mtaani, tutawapiga mtandaoni na tuwapiga kwenye sanduku la kura 2025- Naibu Katibu Mkuu Chadema Bara, Benson Kigaila
SIASA: Tumepeleka malalamiko NEC ya uvunjifu wa kanuni za maadili uliofanywa 8 Oktoba 2020 na mgombea urais wa CCM, John
@MagufuliJP
, aliyetumia shughuli ya kiserikali ya uzinduzi wa kituo mabasi Mbezi, kufanya kampeni ya kwake binafsi na ya wagombea wengine – John Mnyika
Paroko wa Parokia ya Kanisa Katoliki Mt. Yohanne Paul II, Mbezi Mshikamano, Dar es Salaam, Francis Kangwa amefariki na mwili wake kukutwa kwenye tangi la maji nyuma ya nyumba ya mapadri wa Shirika la Missionaries of Africa iliyopo Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph-Posta jijini humo.
Nikiwa Katibu Mwenezi CCM tulikuwa tukitumia uchaguzi wa Local Government kama eneo la kujipima kukubalika kwetu, badala ya kujipima ubavu wetu wa kuwaondoa watu. Kwa hiyo ninachosema, vigezo vinavyotumika kuwawekea watu mapingamizi na kuwaondoa ni vigezo vya kitoto-Nape Nnauye.
Asanteni sana Kilimanjaro. Ninamshukuru Mungu kwa muda wote nilioishi na kufanya kazi Kilimanjaro. Asanteni kwa ushirikiano na mshikamano. Tuendeleze umoja huu na nguvu ya pamoja kwa masilahi ya mkoa na taifa. Nitawakumbuka daima. Mungu awape hitaji la moyo- Anna Mghwira
"Nimezunguka kwenye vituo kadhaa vya kupigia kura. Nilichokishuhudia ni uchafuzi. Siyo uchaguzi" Mgombea Ubunge wa Kinondoni kupitia ACT-Wazalendo, Saed Kubenea
#MwanaHALISIDigital
Acheni tofauti za vyama na mshikamane vema kwa sababu sisi viongozi wa dini mtizamo wetu ni huo. Sisi tunachotaka ni kuleta mabadiliko ya kiutawala, hicho ndiyo chama chetu- Sheikh Ponda Issa Ponda.
PICHA: Nimekutana na huyu kijana hapa (Mrisho Gambo-Mgombea ubunge Arusha Mjini) Safari Bistro cafe... akaomba picha, nikasema ni sawa tu, kwani akose ubunge hata na picha na mimi wajameni...hali yake ni ya majonzi sana – Godbless Lema, mgombea ubunge Arusha Mjini, Chadema
HABARI: Muda wa kuishi una ukomo, kila siku inayopita hairudi, ukimshika na kumweka mtu ndani, huna uwezo wa kumfidia muda huo wa uhuru uliomnyang’anya. Wewe unayemweka ndani si Mungu anayetupa uhai, hivyo makosa yote yadhaminike - Dk. Rugemeleza Nshalla, Rais wa TLS
Huko mitandaoni nawajua mawakili, hata majina yenu ya bandia nayajua na wengine wako ndani ya mahakama, wanamshambulia jaji kwa jina na picha au wakili wa upande wa pili. Tunawafahamu. Siku zao zimekwisha- Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma
Imani kuwa CCM itatawala milele ni potofu, hakuna umilele wa chama chochote kilichoundwa na mwanadamu, CCM itakufa kwa sababu moja kuu, inaamini kwamba haitakufa. Yaani ukiamini hautakufa ndiyo utakufa-Askofu Benson Bagonza.
ONYO: Mbunge wa Mlimba (CCM), Godwin Kunambi amemuonya Mbunge (asiye na chama), Halima Mdee kuacha kuwaita wabunge wapya njuka kwa "lugha za kejeli, lugha za kuudhi ndani ya bunge na sisi wengine ni vijana pia, bado hata umri wa busara haujafika. Namuaonya tu, hamna njuka hapa.”
PICHA: Mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema, Tundu Lissu akisalimiana na Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi ya Karagwe Mkoa wa Kagera, Dk. Benson Bagonza wilayani Kyerwa mkoani humo muda mfupi baada ya Lissu kumaliza mkutano wa kampeni.
#MwanaHALISIDigital
Mimi nilikuwa mjumbe kwenye mkutano uliofanyika Dodoma na hakuna mjumbe hata mmoja aliyesema mchakato wa katiba usubiri hadi mwaka 2025. Baraza la Uongozi linapinga pendekezo la kikosi kazi juu ya suala hili la katiba mpya kusubiri 2025- Profesa Ibrahim Lipumba- Mwenyekiti wa CUF
BONDIA mcheshi nchini Karim Mandonga maarufu kama 'Mtu Kazi' amempiga mkwara mzito mpinzani wake Daniel Wanyonyi raia wa Kenya kwamba amekwenda na ngumi ya kigeni iliyozaliwa Ukraine kwenye midundo ya mabomu. Ngumi inayoitwa Sugunyoo.
HABARI: Katibu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Charles Kitima, amesema, ndani ya miezi miwili iliyopita, “zaidi ya mapadri 25 wamefariki kwa tatizo la kupumua. Masisita na manesi zaidi ya 60. Vifo vinaendelea na tuchukue tahadhari, tusifanye mzaha.”
Kamati ya uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imempitisha Wallace Karia kuwa mgombea pekee kwenye nafasi ya Urais, kufuatia kuenguliwa kwa wagombea wawili ambao ni Evans Mgeusa na Hawa Mninga kutokana na kukosa sifa, mara baada ya kufanyiwa usahili.
HABARI: Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chadema akiwaaga Watanzania waioshio Ubelgiji kwamba anarejea nchini Tanzania Jumatatu ya tarehe 27 Julai 202. Anattarajiwa kutua Dar es Salaam saa saba mchana.
#MwanaHALISIDigital
“Tulipotukanwa na Musiba, watu wakaniambia, Makamba nenda mahakamani. Nikasema siendi, namuachia Mungu. Inshaala, Leo mmeona wenyewe, Mungu amepokea dua za wajawake. Mungu hashibi chakula, anashiba dua na maombi za waje wake.” Yusuf Makamba.
Peter Kibatala, wakili wa upande wa utetezi katika kesi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake watatu, leo Jumatatu ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwamba mashahidi wao watakuwa Lengai Ole Sabaya na IGP Simon Sirro na wengine.
SIASA: NEC ijitokeze hadharani ieleze ni kampuni gani kati ya ile ya Afrika Kusini au ya Dar es Salaam itakayochapisha karatasi za kupigia kura, ieleze kwa umma ni mchakato gani ulifanyika kuipata kwani hiyo ya Dar es Salaam kati ya wamiliki wake wako makada wa CCM – John Mnyika
HABARI: Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika amesema, kikao cha Kamati Kuu cha kuwajadili Halima Mdee na wenzake 18, wanaotuhumiwa kukisaliti kwa kukubali uteuzi wa ubunge viti maalumu kinafanyika asubuhi hii kama kilivyopangwa.
#MwanaHALISIDigital
Kukopa anakosema Spika Ndugai, iwe ni ametuamsha kutoka usingizini, tulichukulie chanya badala ya kulichukulia hasi. Kumtukana tukana tu si sawa, tusimchukulie hasi. Akitamka vile spika anatamka mtu mzima- M/Kiti NCCR-Mageuzi, James Mbatia.
HABARI: Mbunge wa Viti Maalum, Sophia Mwakagenda amesema Rais Samia Suluhu Hassan "anapaswa kutibu majeraha yaliyotokana na uchaguzi mkuu, aachilie wafungwa wote wa kisiasa lakini alikuwa makamu mwenyekiti wa Bunge la Katiba kwa hiyo, aendelee na mchakato Rasimu ya Jaji Warioba."
Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Mkoa wa Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya na wenzake sita kesho Jumatatu, watarejea tena Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kusikiliza kesi nyingine ya uhujumu uchumi yenye mashtaka ya kuendesha genge la uhalifu na utakatishaji fedha inayowakabili.
SHERIA: Mbunge wa Mahonda (CCM), Abdullah Mwinyi, ameshauri sheria zinazokandamiza misingi ya demokrasia na utawala bora, zirudishwe bungeni kwa ajili ya kufanyiwa marekebisho, ili kulinda amani ya nchi.
Nilifanya kosa kwa kutolea mfano wa wakati uliopita badala ya wakati ujao kuwa tusipokuwa waangalifu tunaweza kuchagua viongozi wenye matatizo ya akili, hapo nilikosea- Anthony Diallo- Mwenyekiti wa CCM, Mwanza
" Wengine mmemuona Humphrey Polepole, natoka nje kuna kamera wakati juzi kina Halima wanatoka, kamera hazipo. Nikasema nirudishwe gerezani. Nimwambie Polepole mimi ni mtu ninayejitambua siwezi kununuliwa kwa vipande 30 vya fedha, CCM kinajikanyaga," Mch. Msigwa.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia mkutano wa hadhara kwenye kijiji cha Nandagala wilayani Ruangwa, Mkoa wa Lindi, leo Jumanne. Amewasisitiza waendelee kuchukua tahadhari na kujikinga na corona.
PICHA: Mgombea ubunge wa Kinondoni-
@ACTwazalendo
@SKubenea
akitoa mafunzo kwa mawakala wa
@ChademaTz
, jimbo la Arusha Mjini leo Jumatatu kwenye hoteli ya New Arusha. Wengine waliokuwapo ni Godbeless Lema, mgombea ubunge wa jimbo hilo na Efata Nanyaro, mwenyekiti Chadema Arusha
HABARI: Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa amesema, wamezuia msafara wa Tundu Lissu, mgombea urais kupitia Chadema kuendelea na ziara mkoani humo “tunahofia usalama wake kwani amezuiliwa kufanya kampeni kwa siku saba. Amesema atakaa pale na sisi tutakesha naye”
MAALIM SEIF, LISSU WATUA PEMBA
Mgombea urais wa Zanzibar kupitia ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif na Tundu Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema pamoja na Sheikh Ponda Issa Ponda, wamewasili Pemba kufunga kampeni za Maalim Seif leo Alhamisi.
#MwanaHALISIDigital
Kesi ya jinai iliyofunguliwa na Mwandishi wa Habari, Saed Kubenea dhidi ya aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Christian Makonda itaanza kusikilizwa kesho Alhamisi, Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam mbele ya Hakimu Mkazi, Aron Lyamuya.
Spika wa Bunge, Job Ndugai, amewataka watu wanaopinga tozo ya miamala ya simu, “tupe njia mbadala tutapata wapi fedha. Maamuzi haya tumeyapitisha kwa nia njema, tuwe na Taifa ambalo ni tofauti ili fedha zitakazopatikana zitaenda katika mfuko maalumu utakaowasaidia wananchi.”
Chadema ni chama halali kwa mujibu wa sheria na kinafanya kazi zake kihalali, sidhani ni sahihi kusema chama hiki ni cha watu magaidi. Unakuwa gaidi kama wewe mtu binafsi umedhamiria kufanya matendo ya kigaidi. Nashauri wananchi msome sheria za nchi-Rais TLS, Dk. Edward Hoseah.
Bunge la Bajeti limeanza, nimejiandaa vizuri nitaweka wazi baadhi ya hoja ngumu ikiwemo kuchelewa bwawa la umeme, kukatikakatika kwa umeme, kupanda bei za bidhaa, kuchafuka kwa Mto mara. Tutayasema yote bila kumwogopa mtu, vitisho kutoka kokote- Luhaga Mpina, Mbunge wa Kisesa
LISSU: TUTASHINDA ASILIMIA 65 HADI 75
Mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema, Tundu Lissu amesema, wamefanya mikutano mingi kuliko CCM ambapo wataalamu wao waliofuatilia hali ya upigaji kura “mwelekeo unaonyesha tunashinda uchaguzi huu kati ya asilimia 65 hadi 75.”
HABARI: Chama cha NCCR-Mageuzi kimesema hakikubaliani na matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Jumatano 28 Oktoba 2020 kikidai, miongozo na kanuni za uchaguzi huo ilikiukwa.
#MwanaHALISIDigital
HABARI MPYA: Rais
@MagufuliJP
amefuta tangazo lililotolewa na wizara ya elimu lililofuta mafunzo ya Ualimu ngazi ya Cheti na kuwa ya Diploma kuanzia mwaka 2020/21. Amesema “tangazo hilo ni la kipumbavu limetolewa na wabaya wetu.”
#MwanaHALISIDigital
“Nimesikiliza na kupitia kitabu cha hotuba ya bajeti, ni kirefu… hakieleweki, hata hesabu za kukua kwa kitu zimekosewa, inaonekana waziri wa fedha na watalaam wake wote ni matatizo,” Prof. Lipumba - DAR
Waziri wa maliasili na utalii, Dk. Damas Ndumbaro amesema, Dk. Hamis Kigwangalla, alipokuwa waziri, hakuzingatia sheria wakati anafuta umiliki wa kitalu cha Lake Natron - East, kilichokuwa kinamilikiwa na Green Mile Safaris Ltd. Ameagiza kampuni hiyo, irejeshewe kitalu hadi 2022.
UCHUNGUZI: Tunaendelea na ukaguzi (BoT). Siwezi kusema kilichofanyika hadi sasa tupo site (eneo la tukio), tunaendelea na ukaguzi. - Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere.
MAHAKAMA Kuu, imepokea kesi ya kupinga uchaguzi wa Shirikisho la Mpira Tanzania (TFF) na limemuita, Rais wake Wallace Karia, Bodi ya wadhamini ya shirikisho hilo na mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi kesho Ijumaa, saa 3 asubuhi, kujibu hoja za kwanini uchaguzi huo usisimamishwe.
"Jengine alilofanya Rais
@SuluhuSamia
katika siku 100, ni suala la haki za watu. Alisimamia lakini alituangusha kumchukua Biswalo Mganga kuwa Jaji wa Mahakama Kuu. Ameniangusha sababu hakustahili kuwa jaji kwani kwa miaka mitano akiwa DPP kadhurumu haki zao",-
@fatma_karume
HABARI: Huyu Mungu si hirizi, anataka kila binadamu awajibike na atumie uwezo wake kufikiri. Corona ipo, unaambiwa chukua tahadhari unasema mimi nasali. Mungu wetu anataka watu wawajibike, si kusema tu, tunasali- Padri Charles Kitima, Katibu Mkuu wa TEC
Mbunge wa Geita (CCM), Joseph Kasheku Msukuma leo Jumapili jijini Dodoma, anatunukiwa Udaktari wa Heshima katika siasa na uongozi kutoka Chuo cha Academy of Universal Global Peace cha Marekani. Amesema “hiki ni chuo cha kimataifa na sasa naitwa Dk. Msukuma.”
Aliyewahi kuwa mwanasheria mkuu wa serikali na mbunge wa Baliadi mkoani Simiyu, Andrew Chenge leo Jumatano ofisi ya Lumumba jijini Dar es Salaam amechukua fomu ya kuwania uspika wa Bunge la Tanzania. Amewahi kuwa mwenyekiti wa Bunge.
Shabiki wa Yanga, Mansur Hussen aliyetembea kilomita 1, 400 kutoka Kigoma - Dar es Salaam ameweka vifaa vyake ikiwemo jezi, viatu na track Suit alivyotumia wakati wa safari yake kama kumbukumbu kwenye Makumbusho ya Taifa mbele ya Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Dk Noel Luoga
Rais Samia Suluhu Hassan, akihojiwa na Idhaa ya Kiswahili ya Ujerumani (D.W Swahili), ameizungumzia kesi ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake, akisema “acha waseme tuiachie mahakama itaamua ana kosa au hana kosa, sisi hatuwezi kusema chochote.”
HABARI: Kwanini Spika Job Ndugai anakuwa na usuluba mkubwa sana wa kuwakingia kifua Halima Mdee na wenzake? na anabishana na spika anayeheshimika zaidi kuliko maspika wote wa nchi Pius Msekwa na Msekwa ni mwanasheria, sasa dhana yake ni nini?- Profesa Abadallah Safari, Wakili
"Bashiru na chama chake wanachukua wapigiwa kura badala ya kuchukua wapiga kura, kama una akili zako timamu mtu unapataje presha? ndio maana unaona watu hatushtuki shughuli zinaendelea kama kawaida," Joseph Mbilinyi (Sugu), Mbunge wa Mbeya (Chadema).
"Kama Bunge halisemi haya sisi tutayasemea ...kama wabunge tuliowachagua hawatekelezi wajibu wao hata wakituita wachochezi kama kutuweka jela watuweke tu. Afadhali uhukumiwe duniani kuliko kuhukumiwa mbinguni," DK. SLAA
Nimezungumza na TAKUKURU na wameweza kufuta kesi 147 ambazo waliwabambikizia watu mbalimbali huko, na nyie Jeshi la Polisi jikagueni kama mnazo za aina hiyo zifutwe. Ili tupunguze wingi wa mahabusu kule kwenye majela yetu-Rais Samia Suluhu Hassan.