The Permanent Secretary of Culture, Arts and Sports. Former Chief Government Spokesperson of Tanzania and Former Director of Presidential Communication.
Nimefurahi kukutana na huyu mwamba kabisa wa Gunners.
Long live Arsène Wenger and thank you for your invaluable contribution to soccer especially uplifting African Footballers.
Mhe. Rais Magufuli ampa zawadi ya Tausi Mhe. Rais Uhuru Kenyatta kama kumbukumbu ya uhusiano mzuri, undugu, urafiki na ujirani mzuri wa Tanzania na Kenya.
Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli amempigia simu na kumpa pole Mhe. Zitto Zuberi Kabwe aliyepata ajali ya gari jana Mkoani Kigoma. Amemuombea heri ili apone haraka na pia amewashukuru Madaktari na Wauguzi wa Kituo cha Afya cha Kalya na Hospitali ya Maweni kwa matibabu waliyompa.
Hujawahi kutuangusha Watanzania, leo tena unatuheshimisha na tunamuomba Mwenyezi Mungu asimame na wewe na asimame na Watanzania. Tuzo ya BET ije nyumbani.
Kila la Kheri
@diamondplatnumz
#betawards
Happy Birthday Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli🎂.
▪︎Mwenyezi Mungu akupe umri mrefu, afya njema na Maarifa zaidi.
▪︎Watanzania tumekuelewa, tunakushukuru na tupo pamoja.
▪︎Tanzania Mpya tunaiona na tunaiishi.
#HapaKaziTu
====TAARIFA====
Mhe. Rais Magufuli leo tarehe 20 Oktoba, 2019 atawaapisha Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI na Balozi.
Hafla ya uapisho huo itafanyika Ikulu Jijini DSM kuanzia saa 9:30 alasiri hii. Itarushwa mubashara kupitia Redio, Televisheni na Mitandao.
HISTORIA
Picha hii imetoka kwa Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Mzee Philip Mangula. Inaeleza kwa mara ya kwanza Baba wa Taifa alipofika Chamwino Mkoani Dodoma na kuanzisha Ikulu mwaka 1971.
Serikali HAIJALIPIA kuweka tangazo la Tanzania katika jengo refu kuliko yote Duniani liitwalo Burj Khalifa lililopo katika Jiji la Dubai.
:
Tangazo hilo limewekwa kwa lengo la kuitangaza Tanzania kutokana na uhusiano mzuri uliopo kati ya nchi yetu na Umoja wa Falme za Kiarabu.
CHUMA KIMESHTUKA!!!
Makanisa, Masinagogi na Misikiti ya Marekani ifunguliwe kuanzia wikiendi hii - Rais Donald Trump
Tunahitaji zaidi maombi wakati huu.
HAPO VIPI?, HAPO VIPI?, HAPO VIPI????
Nimefurahi kukutana na Mzee wangu, Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mhe. Alhaji Ali Hassan Mwinyi kando ya Dhifa ya Kitaifa Ikulu Jijini Dar es Salaam.
:
Anasema leo asubuhi amepiga zoezi kwa kutembea kwa miguu kilometa 5 na yupo fiti.
Mzee Ruksa hoyeeee!!!!!
Tanzania yatoa msaada wa Dola za Marekani 1,000,000 kwa Uturuki kufuatia madhara ambayo nchi hiyo inepata kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea mwezi Februari mwaka huu.
Tayari Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC) imemteua Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kugombea kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM na Mhe. Samia Suluhu Hassan ameteuliwa kuwa Mgombea Mwenza.
Mhe. Rais Kenyatta alimtembelea Mhe. Rais Magufuli nyumbani kwake Chato Mkoani Geita na kumjulia hali Mama Mzazi wa Mhe. Rais Magufuli, Bibi Suzana Magufuli.
ALHAMDULLILAH!!! 🙏🏼🙏🏼.
Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa baraka zake na kunisimamia daima.
Namshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuniamini na kuniteua katika jukumu hili la Katibu Mkuu. Kwangu hili ni deni, naahidi kulilipa kwa utumishi uliotukuka.…
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 16 Juni, 2020 atalihutubia na kulifunga Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia 4:00 asubuhi hii. Matangazo yatarushwa Mubashara na Redio, TV na Mitandao.
PIPA LANYANYUKA MAREKANI.
▪︎Ni Boeing 787-8 Dreamliner ya pili.
▪︎Kutua Dar es Salaam kesho saa 8:00 mchana.
▪︎Kupokelewa na wananchi wakiongozwa na Mhe. Rais Magufuli.
#HapaKaziTu
#TUELEWANE
Serikali ya Awamu ya Tano yanunua Boti ya Wagonjwa kwa ajili ya kuhudumia wananchi wa Ukerewe. Imegharimu shilingi Milioni 200 na ina uwezo wa kutumia dakika 30 kusafiri kati ya Ukerewe na Mwanza.
Hongera Rais Magufuli, Hongera wananchi wa Ukerewe.
#HapaKaziTu
JPM safarini kutoka Chato, awasalimu wananchi wa Singida. Wampongeza kwa kazi nzuri.
• Azungumzaye ni Aboubakar Francis Kisike, Mkazi wa Singida.
#HapaKaziTu
Ndege yetu aina ya Bombardier Q400 iliyokuwa imezuiliwa nchini Canada ilikwishaondoka Canada kuja Tanzania. Aidha, ndege kubwa nyingine 3 (2 Bombardier CS300 kutoka Canada & 1 Boeing 787-8 Dreamliner kutoka Marekani) zitawasili baadaye mwaka huu. Nawatakia Ijumaa Kuu njema.
KUMEKUCHA!!
JPM achukua fomu za kuomba ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kugombea kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadaye mwaka huu 2020.
Tunawashukuru na tunawatakia kila la heri Madaktari, Wauguzi na wafanyakazi wote waliomstari wa mbele katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona (Covid-19). Mungu ni mwema TUTAVUKA.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli atazungumza na Viongozi wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama kuhusu hali ya ugonjwa wa Corona. Matangazo ya kikao hicho yatarushwa mubashara kutoka Chato Mkoani Geita kuanzia saa 9:45 alasiri leo Aprili 22, 2020.
Ni uchungu mkubwa kuwapoteza Joseph Kambanga “Jenerali” (Meneja TEHAMA - TBC) na Lutengano Haonga (Mwandishi wa Habari Mwandamizi - TBC). Ni mtihani mzito kwa wana familia wenzangu wa TBC.
Laleni salama Kaka zangu, kamwambieni Marin Hassan kuwa ARIDHIO inachanja mbuga.
Mhe. Rais Magufuli leo Machi 25, 2019 atakutana na wachezaji wa Taifa Stars, Viongozi wa TFF, Kamati ya Uhamasishaji na Bondia Hassan Mwakinyo Ikulu DSM. Atawapongeza na kula nao chakula cha mchana. Tukio litarushwa Live! na Redio, Televisheni na Mitandao kuanzia saa 4:00 asubuhi
AKITROTI.
Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli na Mama Janeth Magufuli wamkaribisha Mhe. Edward Ngoyai Lowassa na Mama Regina Lowassa, Ikulu Chamwino, Mkoani Dodoma.
Mhe. Rais Magufuli leo Mei 21, 2020 atawaapisha viongozi mbalimbali aliowateua hivi karibuni. Tukio la kuapishwa kwa viongozi hao litarushwa moja kwa moja kutoka Ikulu, Chamwino Mkoani Dodoma kuanzia saa 3:30 asubuhi hii kupitia vyombo vya habari vya Redio, TV na Mitandao.
UFAFANUZI.
Tsh. Bil. 4 za Sherehe za Uhuru zilizotumika kujenga barabara ya Morroco-Mwenge (2016) zilifanya upanuzi wa barabara za njia 2 zilizopo katikati ya barabara na Tsh. Bil. 71.8 za msaada wa Japan zimetumika kujenga barabara za njia 4 zilizozinduliwa na Mhe. Rais Samia.
JPM avuka Daraja la Mkapa (katika mto Rufuji) lenye urefu wa meta 970 kwa miguu, kumkumbuka Hayati Benjamin William Mkapa aliyejenga daraja hilo wakati wa uongozi wake.
Welcome back KLM.
Tanzania is safe and blessed. Come one, come all and ENJOY YOUR STAY IN THE LAND OF KILIMANJARO, SERENGETI AND ZANZIBAR.
#TanzaniaUnforgettable