Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akiwarejesha ng’ombe wake kutoka malishoni wakati wa mapumziko ya mwisho wa wiki jimboni kwake Kongwa Mkoani Dodoma.
"Tumesikitika zaidi kwa kuwa matamko haya ya dharau yametolewa na CAG akiwa huko Marekani. Ni utamaduni wa kawaida kila anayesafiri kutoisema vibaya nchi yake wala Taasisi muhimu kwa nchi" alisema Spika wakati akizungumza kuhusu kauli za kudhalilisha Bunge alizotoa CAG.
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (Mb), leo tarehe 7 Jan, 2019 saa 7.00 mchana ataongea na Waandishi wa Habari Jijini Dodoma kuhusu kauli za kudhalilishaji Bunge zilizotolewa na Prof.Mussa Assad, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na Mhe. Halima Mdee, Mbunge wa Kawe.
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai amelieleza Bunge kuwa amepokea taarifa ya ukaguzi wa hesabu za Ofisi ya CAG na anaiwasilisha Kamati ya PAC ili iweze kufanyiwa kazi
Spika wa Bunge, Naibu Spika na Katibu wa Bunge wakifurahia jambo na Ndg. Peter Mollel alimaarufu kama Pierre Liquid Jijini Dodoma, kabla ya kumualika kutembelea Bunge.
WITO KWA WADAU KUTOA MAONI KUHUSU AZIMIO LA BUNGE KUHUSU MAPENDEKEZO YA KURIDHIA MAKUBALIANO KATI YA SERIKALI YA TANZANIA NA DUBAI KUHUSU UENDELEZAJI NA UBORESHAJI WA UTENDAJI KAZI WA BANDARI TANZANIA
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (katikati) akiagana na Mbunge wa Misugwi Mhe. Charles Kitwaga katika Uwanja wa Ndege wa Jijini Dodoma kabla ya kusafirishwa kwenda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi
Spika wa Bunge Mhe. Job Y. Ndugai (Mb) atazungumza na Waandishi wa Habari jambo muhimu kuhusu Bunge, kesho Jumapili tarehe 14 Aprili, 2019, saa sita na nusu mchana, katika Ofisi Ndogo ya Bunge Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwasilisha Mapendekezo ya Serikali ya Mpango, Kiwango na Ukomo wa Bajeti kwa mwaka wa Fedha 2021/22 katika Ukumbi wa Pius Msekwa Jijini Dodoma
Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali Prof. Mussa Assad akiwa mbele ya Kamati ya kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kufuatia kauli za kudhalilisha Bunge alizozitoa akiwa nje ya nchi.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akikagua ukarabati wa jengo la Bunge leo Jijini Dodoma. Pamoja nae katika ukaguzi huo ni Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai, Wakurugenzi na Maafisa wa Ofisi ya Bunge na Mahandisi wanaofanya ukarabati huo.
Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) ambaye pia ni Spika wa Bunge la Tanzania na Mbunge wa Mbeya mjini
@TuliaAckson
akiwa amepakatwa na Mama yake mzazi Bi. Nkundwe Mbonile akimpongeza kwa Ushindi wa Urais wa IPU baada ya kumtembelea nyumbani kwake Rungwe Mkoani Mbeya leo
Waheshimiwa Wabunge wapatiwa tablets kwa ajili ya kuwasaidia katika matumizi ya shughuli za Bunge lengo likiwa ni kuondoa matumizi ya karatasi. Zoezi hilo limefayika siku moja kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Kumi na Saba wa Bunge Jijini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai amemwandikia barua Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kumtaarifu kuwa Jimbo la Singida Mashariki lipo wazi kufuatia aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Lissu kutokuwepo bungeni bila taarifa, na pia kutojaza fomu ya tamko ya mali na madeni.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai amewaomba radhi Watanzania na watu wote walioguswa na kauli yake kuhusu mkopo wa fedha za uviko-19 akisema alinukuliwa vibaya na kwamba hana ugomvi na Rais Samia Suluhu Hassan kwani ni mtu anayefanya kazi kwa maslahi ya Watanzania.
Spika Ndugai ambaye pia ni Mbunge wa Kongwa akivalishwa vazi rasmi la jadi la uchifu na kupewa mbuzi na wazee wa jadi kama ishara ya heshima katika Kijiji cha Nghumbi kilichopo wilaya ya Kongwa. Spika anatarajia kutembelea vijiji kumi na mbili katika Wilaya ya Kongwa.
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai amesema kuwa Bunge limesitisha uwakilishi wa Mhe. Stephen Masele (Mb) katika Bunge la Afrika hadi Kamati ya Maadili itakapomhoji kuhusiana na tuhuma za kinidhamu zinazomkabili.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), ameibuka mshindi kwenye mbio za mita 100 zilizoshirikisha Viongozi Wanawake wakati wa tamasha la CRDB Bank Pamoja Bonanza katika Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma leo Juni 25, 2022.
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akiosha magari tofauti tofauti wakati wa shughui ya kuosha Magari kwa ajili ya kuchangia fedha za kujengea Vyoo vya mfano kwa ajili ya watoto wa Kike na wenye mahitaji maalum. Shughuli hiyo imefanyika katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma
Mkutano wa Kwanza wa Bunge la 12, umeanza kwa kumchagua Mbunge wa Kongwa, Mheshimiwa Job Yustino Ndugai (Mb) kuwa Spika wa Bunge hilo kwa kura 344 kati ya kura 345 zilizopigwa ushindi ambao ni sawa na asilimia 99.7.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akiongoza kikao cha kamati ya Uongozi kilichokaa kujadili taarifa ya maandalizi ya ujio wa Rais, utaratibu wa kuingiza viongozi mashuhuri ndani ya ukumbi wa Bunge na mabadiliko ya ratiba ya Mkutano wa tatu wa Bunge.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, tarehe 11 Novemba, 2023 ameshiriki matembezi ya Jeshi la Polisi yenye lengo la kumpongeza kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU)
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mgombea Urais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) Mhe. Dkt. Tulia Ackson, akiendelea na zoezi la kujinadi kwa Wajumbe katika kampeni ya Uchaguzi unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Oktoba, 2023 Luanda nchini Angola.
Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya M. Kikwete atembelea Banda la Bunge katika Maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Kambarage Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akizungumza Bungeni kuhusu madai ya Mhe. Tundu Lissu kuwa Ofisi ya Bunge haijawahi kumjali kifedha tangu alipopata matatizo.
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akipita katika mashine maalum ya kunyunyuzia yenye dawa ya kujikinga na ugonjwa wa Corona wakati alipoingia kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma.
Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai (Mb), akipokea msaada wa kompyuta kutoka kwa Balozi wa China Nchini Tanzania, Mheshimiwa Wang Ke.Msaada huo wa Kompyuta umetolewa na Bunge la China kwa Wabunge wa Bunge la Tanzania.
Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, akiwa katika picha ya pamoja na Mtoto Barka Seif Mpanda (8) nje ya Ukumbi wa Bunge Jijini Dodoma, Mtoto Barka ni Mtanzania pekee aliyeanza kucheza mpira wa miguu akiwa na umri wa miaka minne (4) na kupata mafanikio katika umri mdogo.
Spika wa Bunge anatafakari hatua za kinidhamu atakazomchukulia Mbunge wa Kilombero Mhe. Peter Lijualikali kufuatia kauli za kejeli dhidi ya Bunge alizozitoa wakati akizungumza na Waandishi wa Habari tarehe 17 Machi, 2018
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai amesema kuwa leo asubui amepokea barua ya kujiuzulu Ubunge wa Jimbo la Ukonga kutoka kwa Mhe. Mwita Waitara na hivyo atamwandikia barua Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ili aweze kuendelea na taratibu zingine.
Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson amewasili Jijini Luanda, Angola kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa 147 IPU. Katika Mkutano huo pamoja na mengine utafanyika Uchaguzi wa Rais mpya wa Umoja huo ambapo Dkt. Tulia ni miongoni mwa Wagombea.
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisi Ndogo ya Bunge Jijini Dar es Salaam kuhusu ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2017/18 .
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akiongoza kikao cha Kamati ya Uongozi ya Bunge hii leo kama sehemu ya maandalizi ya kuanza kwa Vikao vya Mkutano wa tatu wa Bunge la Kumi na mbili vinavyotarajiwa kuanza siku ya Jumanne tarehe 30 Machi, 2021 Jijini Dodoma.