Mwanamke usifute namba yake wala usim'block. ILA USIMTAFUTE.
Mfanye ajue kuwa unauwezo wa kumfikia lakini umechagua kutofanya hivyo..
Wanachanganyikiwa sana wakigundua wanapuuzwa kuliko ukiamua kushindana nao..
Sipendi kukagua simu ya Mwanamke, sipendi kumfatilia sana Mwanamke, napenda aishi kwa akili yake , afanye vitu kwa utashi wake, na siku akishindwa basi ashindwe kwa hekima zake..
Ni mahusiano kwangu sio utawala.. ni mapenzi sio biashara..
NI NGUMU KUMCHUNGA BINAADAMU.
Wale tuliokuwa tukiwaona wasumbufu, wameacha kutujulia hali.
Tuliokuwa tunadhani wanajipendekeza, wapo bize na maisha yao.
Tuliowaona wajinga kila walipotusamehe, wamechagua watu wapya wa kuvumilia madhaifu yao.
Never take love for granted. Hata hisia imara huisha, zikipuuzwa.
“Mlipe mtu ujira wake kabla jasho lake halijakauka. Hata kama ni kiwango kidogo cha pesa basi angalau usizidishe muda ulioahidi kumlipa. Na kama ukikumbwa na changamoto za kutimiza ahadi yako onyesha kuwajibika."
Ushauri nilipewa na Mlinzi wa shule flani..
Vijana wenzetu mliopata bahati ya kuaminiwa mahala flani, kuweni mabalozi wetu wazuri.
Usela, ujuaji, uwe na mipaka wanangu, msiharibu.
Kiasi cha kuwafanya waliowapa nafasi watutazame vijana wote ndio WALEWALE..
Tabia zenu, zimebeba kesho za vijana wenzenu,
Kisasi chake yeye ni kulala na wanaume tofauti..
Kisasi chako ni kufanikiwa.
Kisasi chake kinampunguzia thamani.
Kisasi chako, kitatengeneza kesho yako.
Uzuri huisha, mafanikio hudumu. Jijenge braza.
Yeyote anayekupa connection ya kupiga pesa, Automatically anakuwa tayari ni familiaa..
Yeyote anayekupa mipango ya kupata ugali, Moja kwa moja anakuwa damu yako.
Tuwalinde watu wa aina hiyo, maana ni adimu sana.
Huyu ndiye mwanaume.. Akiwa mtoto anampenda sana mama yake..
Akiwa kijana anampenda sana 'Girlfriend' wake..
Akiwa baba anampenda sana mtoto wake.
Akiwa babu anampenda sana Mjukuu wake.
YES, hakunaga penzi la kudumu kwa mwanaume.
Philippians kinajulikana kama kitabu cha furaha zaidi kwenye bible..
Lakini kiliandikwa gerezani,
Cha kujifunza hapa, ni hali yako haipaswi kuiba furaha uliyonayo.
Unaweza kupitia mateso na bado ukazalisha tabasamu kwa wengine.
Baada ya mvua kuacha kunyesha, mwamvuli hugeuka mzigo.
Baada ya kipofu kupona, fimbo yake hukosa maana tena.
Ni ngumu watu kukupenda wakishamaliza kukuhitaji. Ni maisha.
Siku Moja chukua CV yako, kisha angalia sehemu ya Referee wako, wapigie simu jifanye kama wewe ni mkurugenzi wa kampuni unataka kujua kuhusu wewe, usikie maoni yao..
Unaweza kuta mchawi wa maisha yako yupo kwenye CV yako..🤷
Kuna ambao bila ugomvi wala chuki, walifuta namba zetu.
Waligundua mapenzi yamekwisha na hatuwezi kuliongelea Hilo, wakachagua kujiongeza.
Wamebaki kuwa ma ex tunao heshimiana na kupendana ila kwa mbali sana.
Maturity..❤️
Nilianza kuwa na adabu Ile siku niliyoona engine ya Benz ikiwa imebebwa kwenye mkokoteni inaenda kuuzwa kama skrepa.
Niliogopa pale msiba wa yule tajiri kaburi lake kuchimbwa na wale vijana wanaoitwa wezi na masela wa mtaani.
Maisha yakikupa ukubwa, chagua kuwa humble.🙏
Tumechoka ndio, lakini ndoto zetu tumuachie nani?
Tunalala hoi tunamka hoi hadi wachawi wanaweza kutupeleka shamba na bado tukategea kulima.
Tunawaza mengi huku tukijipa imani, labda kesho haitokuja na adhabu nyingi kama leo.🙏🥲
Kuna dogo kaweka status, kumekucha tukapambane, Afu yeye karudi kulala.
Kuna binti kaandika, beautiful night with bae, na jana alikuwa analia kwa kutopokelewa simu na bwana ake!
Kuna jamaa kapost Aya za Biblia, na sasa yupo njiani anakwenda kwa Mganga
Mtandaoni usije na wivu💔
Kuhusu mimi. Utanikuta kanisani, mbele kabisa naimba mapambio,
Na bado utaniona club, pale counter nacheza amapiano..
Kitu kizuri ni sina muda wa kujieleza kivyovyote kwako..
Mi ni malaika ama shetani? Utajua mwenyewe na tafsiri yako..
Mpenzi wako aliyekueka dp, tumemtongoza na amekubali.
Yule binti yako unayemchunga kwa kujenga fensi, ana ujauzito na baba wa mtoto hamjui.
Yule uliyetambulishwa ni just a friend, wewe ndo rafiki yao wakiwa pamoja.
Uaminifu ni hulka ya mtu sio kiwango cha kuchungwa kwake.
Oya mbabe, yule mnyonge uliyemwambia akashtaki popote, ameenda kulia kwa Mungu wake
Yule uliyegombana nae ukamwambia ukifa asikuzike, ametangulia yeye mbele za haki na ugomvi wenu
Yule uliyekwenda kumsema vibaya kwa watu, ndie huwa anakutetea wakati haupo.
UNAJISIKIAJE BINGWA?
Inua kichwa mwanangu, kaza.. kama unasubiri neno zuri la kukupa tumaini, hautalisikia Kamwe.
Wewe ni mwanaume, hakuna anayejali kuhusu wewe, hakuna anayekuhitaji..
Mpaka pale utakapokuwa na hela ama chochote cha kuongeza thamani kwenye maisha yao..
Kaza.
Ni wajibu wake kuvunja mahusiano na wewe kama ana mashaka na mafanikio ya kesho yako..
Ni jukumu lako kumfanya ajutie maamuzi yake, mpaka mwisho wa maisha yake..
Pambana msela.
Kuna tofauti kubwa sana kati ya,
Mwanamke anayetaka kuwa na mume.
Na mwanamke anayetaka kuwa mke.
Kama unadhani wanafanana, basi una safari ndefu sana..
Mfundishe kijana wako kazi za nyumbani, hili kesho aoe mke sio mtumwa
Mfundishe binti yako nidhamu ya pesa, hili kesho aolewe na mume sio mhasibu
Wafundishe kuhusu makosa na samahani, kesho wajue wanaenda kuishi na binadamu sio malaika
Wafundishe mapema, ulichochelewa kukijua.
Na wakikuuliza kuhusu mimi? Wajibu mchizi hakujipata, kwasababu ya kiburi chake
Waambie alirudi kijijini na maisha ni magumu zaidi ya mwanzo
Kula yangu ni ya shida, Sina muda wa kuiwaza kesho, na naishi na laana ya wazazi.
Waambie kwasababu Habari zetu mbaya ndio furaha yao,😢
Wakati mwingine unatakiwa umuache huyo mwanamke akawe pasua kichwa kwa mwanaume mwingine..
Wakati huo wewe unamsubiri mwanamke atakayekuwa amani kwenye maisha yako.
Zaliwa. Nenda shule. Tafuta kazi. Funga ndoa. Pata watoto. Fata sheria. Teseka. Kisha kufa.
Maisha yetu tayari yapo programmed, muda wote tupo bize kukimbizana na kitu flani..
Tunasahau kuishi. A SAD STORY.
Stage tuliyofika, ukija kuthibitisha ubaya ulioambiwa kuhusu sisi, tutakwambia amini ni ukweli huo.
Ukituambia fulani anatusema mno, tunakujibu hata sisi huwa tunamsema hasipokuepo.
Tumeacha kujisafisha kwenye kila tuhuma, kwasababu ukweli wetu kwenu ni, JAMAA ANAJITETEA SANA.
Kama una mtu mwenye nia njema na wewe, anayeweza kukukataza unapokosea, na kukushika mkono wa wapi ni uelekeo sahihi. Hongera.
Sisi wengine ulimwengu ndio ulikuwa mama, vyote tulivyojifunza vina historia ya maumivu yetu.
Ilibidi tujikwae sana, ili tufike unapotuona.
Muda mwingine hatutoki kitandani. Sio kwasababu ya usingizi na uchovu.
Bali ni msongo wa mawazo, vichwa vyetu mpaka sasa vina maswali ya kivipi tutarudisha tabasamu nyumbani.
Ni kwa vipi tutarudisha jasho na sacrifice walizofanya wazazi wetu kwaajili yetu.
Inatu'umiza sana.😢
Kitu kimoja nawakumbusha wanangu, Gawana na wenzio ridhiki Ili ipunguze chuki..
Ama ficha sana neema zako, Ili uikimbie husda..
Watu hawapendi uwe na raha, kama una kazi, mpenzi mzuri, hela na chochote cha kutamaniwa, ficha.
Wengi wameharibikiwa kwasababu ya hasadi🙏
Chochote unachofanya, Tafadhali!
Usikanyage ugali wa mtu,
Usizamishe boti ya mwengine, usichukie kutangulia kwa yeyote.
Kwasababu, keki ya Taifa ni kubwa, bahari ina kina kirefu cha yeyote kuogelea upande wake, na foleni ya riziki yako haiitaji haraka ama kuchelewa kwa wengine.
Vitu unavyovifanya saivi ukidhani ni ujanja, Kuna mtu ndo anajaribu kuacha. Maana vimem'cost sana
Yale mambo unayoyaita ndio ujana, kuna kijana amekubali yampite.
Chunga mstari uliopo kati ya kula maisha na kuharibu kesho yako.
Leo yako ndo itaamua uzeeni ucheze bao au golf ⛳
"Mama amesema umpe Unga kidogo akipata hela atarudisha"
"Baba J akija kuniulizia mwambie sipo"
Hizi kauli mbili kutoka kwa wazazi wetu, zilibeba maumivu mazito..
Kuna wakati unaweza kuhisi unayopitia ni adhabu, kumbe ndio MAISHA YENYEWE 😢
Jogoo aliekuwa akionekana mwema kwa kuwaamsha mapema, kachinjwa walipo kuja wageni.
Sukari iliyosifiwa utamu kwenye chai, usiku imetelekezwa ni zamu ya chumvi.
Pamoja na mbwembwe zote za suti kupendeza, mazishi yalihitaji sanda.
Unaweza kuwa muhimu lakini sio kila wakati..🙏
Na machozi yako yajayo yasiwe kwasababu ya anguko na maumivu..
Bali ni baraka na maombi yaliyojibiwa..
Na furaha yako ijao iwe real, na sio Ile unayoionesha ili wanaokutegemea wasife moyo.
AMEIN🙏
Gari la ndoto zako, kuna mtu analiendesha baada ya kuamka
Yule mwanamke wako asiye na muda, Kuna msela anamuona kero
Yule ex wako mpiga vizinga, Kuna sehemu anamvumilia mwana asiyempa chochote
Yule anayekuvimbia, Kuna sehemu na yeye wanampuuzia
Dunia Haina mbabe wa kila mtu🙏
Maumivu makubwa ni kufuta namba ya marehemu.
Maumivu makubwa zaidi ni pale unapokutana na conversation yenu, nyakati zile yu hai..
Zile emoj za kucheka, namna anavyo reply status zako, na utani wa hapa na pale..
Ooh, Kifo.😢
Usimtengenezee gereza.. muache kijana mdogo akawinde.
Hiki ndio kipindi ambacho ana nguvu ya kupambana kwaajili ya kesho yake, mruhusu akawinde.
Kama akimuua tembo, umasikini wake utaisha.
Kama tembo atamua kijana, umasikini wake utaisha vilevile..
Ni maisha.
Kuna ambao hawaongei tena na sisi, wakituona barabani wanabadilisha njia. Wanajistukia
Walitukosea wakadhani hatutajua, na wala hatukuwaambia, ila wakajipunguza maishani mwetu
Mpaka leo wanatamani kutusahau, lakini Wema tuliowatendea bado unawatesa moyoni.
Sisi Bado tunaishi🙏
Mwanamke anamkinai haraka sana mwanamme ambaye hana vile vitu alivyotarajia amkute navyo nyakati zile anamtongoza.
Imagination imewaingiza watu wengi kwenye mahusiano, lakini uhalisia umefanya mapenzi mengi yavunjike.
Kuna muda tunacheka tukikumbuka zile siku tulizolia bila tumaini.
Na kuna nyakati tunalia kwa kukumbuka zile siku tulizofurahi kweli..
Maisha yamenifundisha kuheshimu nyakati.🙏
Mwambie Mungu shida zako, yeye hato screenshot.
Lia na malaika wako, wao hawataenda kukutangaza kwenye ma group usiyokuepo..
Mnyenyekee aliyekuumba, yeye hatokuona chawa wa mtandaoni..
Usiwafurahishe wanaopenda maumivu yako.
Mwanamke hatongozwi Dingi lai.
Jali vipaumbele vyake, yeye ajali hisia zako.
Mfanyie hisani, yeye atatafsiri ni upendo.
Wanawake Wana huruma? Ni kweli.
Nathibitisha haya nikikumbuka story ya muuza nyama, aliyetunukiwa penzi kwasababu ya kumuongezea mfupa.
HISANI.👍
Baada ya kukaa chini na kutafakari mbona mambo yetu hayaendi, tuligundua bado tuna vinyongo vya nafsi.
Tuligundua wale waliotukosea bado tulikesha kuwaombea mabaya..
Sasa tumechagua kuwa weupe wa roho, tumesamehe waliotukosea..
Sasa hatuna tena mizigo ya chuki moyoni..🙏
Uwezo wa kutatua shida zangu bila kumsumbua yeyote.
Moyo wa kupokea maumivu hata kutoka kwa wale ninaowaamini.
Nafsi ya kukinai nisichoweza kumiliki.
Afya isiyonikweza mbele ya wagonjwa, mafanikio yasiyonijengea kiburi.
Na mwisho mwema, baada ya pumzi zangu. Mungu nisaidie🙏
Kuna tofauti kubwa kati ya niliteseka nae, na nilikua nae wakati anateseka.
Tofauti kati ya nilimvumilia mno na nilibaki nae kwasababu nampenda.
Mwanamke akiamua kuelezea ushindi wako, ikumbuke historia yenu..
Kwa bahati mbaya maisha hayakusubiri uwe sawa..
Unapaswa kujiponya nyakati ambazo unakutana na vidonda vipya.
Unapaswa kujisamehe muda ambao unafanya makosa mengine pia.
Aliniambia John Lennon, maisha ni kile kinachotokea pale unapokuwa bize kupanga vitu vyengine..
Uwezo wa kusema SINA pale unapoombwa kilicho juu ya uwezo wako..
Uwezo wa kuishi ndani ya kipato chako bila kuogopa kuitwa bahiri.
Kuruhusu mambo mengine ya kupite, kwa kuepuka sifa za kijinga.
Sio uchoyo/ubinafsi bali ni kuishi kwenye bajeti na mfuko wako..
Maisha yanataka uwe muongo mbele ya wasiopenda hatua zako..
Yanataka uwe muigizaji kwenye maisikio yanayokutangaza ubaya.
Yanahitaji uwe loyal kwa wenye huruma na harakati zako..
Vinginevyo na hapo maisha ya pretend, hayatakusaidia..
Mungu alimpa nafasi Israel awe malaika mtoa roho, lakini alimnyima Nabii Mussa kuwa mtoa riziki
Kama tunadhani kifo ni fumbo,
Basi kupata na kukosa kwetu ni zaidi ya mtihani.
Imefichwa siri kubwa sana kwenye kupata fungu letu.
Ndio maana, kifo kina tafsiri ya mwisho wa riziki.
Unapoenda kulala leo usiku mwambie Mungu, Jua linapozama ninakuomba likazame na yote yaliyoniumiza Leo.
Nimeweka kila maumivu na uchungu mikononi mwako..
Ili kesho nianze siku yangu nikiwa na furaha na nguvu mpya..
Amein 🙏
Aliyesomea sheria kesi yake ya kwanza kuisimamia huku uraiani, mteja wake amehukumiwa kifungo cha maisha jela.
Mdada aliyekubali kuolewa na Mzee Ili arithi Mali, ametangulia kufa yeye.
Kitaalamu inaitwa, ANGUKO LA MATAMANIO.
Kuna mahala yule rafiki yako, kaulizwa kuhusu uwezo wako, kajibu "Huyo muacheni, atawaharibia
Kuna sehemu yule twin wako anamwambia mpenzi wako jinsi ambavyo hujatulia
Yule best yako anayekwambia muamini Mungu, amekuendea kwa Mganga
Kwenye kila rafiki kuna Adui unayemkumbatia.
Inakuja siku, Wasiotujua, majibu ya Dua zetu wataita BAHATI.
Wasiotufahamu, matokeo ya jasho letu, watasema TUNABEBWA.
Wasiotupenda, riziki itakapokuwa upande wetu baada ya msoto, watahusihanisha na USHIRIKINA.
Wasichokijua ni Mungu ndie aliyeshika kalamu ya ndoto zetu.🙏
Asanteni wanawake wote mnaotuelewa..
Hamtupi presha ya ndoa, kwasababu ya sauti za mtaa kuwa umri unaenda..
Mnaishi kwenye kipato Chetu kidogo, bila kujali post za bata za rafiki zenu..
Na kubwa kuliko mnaheshimu kinachotupa riziki, Asanteni mno.❤️🙏
Kuna waliotukosea wanajishtukia kwenye kila hatua zetu.
Status zetu wanajiona wao, story zetu wanahisi tunawalenga wao.
Simu zetu hawaokoti, na wao hawatupigii, kwasababu hawana cha kutueleza.
Wanaishi kwenye gharama ya kuvunja uaminifu tuliowapatia..
Maisha baada ya shule, kuna walio olewa/oa, kuna wenye mishe, na wanaoendelea katafuta tobo.
Kuna waliokwenda nje ya nchi, Kuna waliorudi kijijini kulima
Ukizungumza na classmate wako, chagua kuwa muoga, mpongeze kwa kubaki hai mpaka sasa
Maisha si rahisi kwa kila mmoja wetu🙏
Kuna makofi utapigiwa yakimaanisha maliza kuongea.
Kuna pongezi utapewa zikimaanisha endelea kupotea.
Kuna zawadi utatunukiwa, zikimaanisha endelea kubweteka.
Ukiwa mtu wa kuongozwa na sifa, Kuna watu watakutumia
Sifa zikiishi kichwani, majivuno yataishi moyoni. Kuwa makini🚨
Jana wakati natoa salamu zangu za mwisho kwa Gardner, Captain.. nilijifunza vingi sana kuhusu kifo.
Lakini ilinitafakarisha sana pale nilipomuona kipofu, nae kaja kuaga..
Hapo ndipo nikathibitisha, Wema ni lugha ambayo kiziwi husikia, na kipofu huona..
Wema ni akiba ya kweli🙏
Hatukuwahi kuwaombea
yawapate mabaya kama yetu, ingawaje walituona sisi wazembe
Hatukuwahi kufurahia anguko lao, japo walituita wajinga
Mitihani ya Mungu na wao wakapitia majaribu kama yetu
Na sasa ndo wanajua kumbe sio swala la jitihada na akili, kuna muda inatangulia bahati
We bado sio mbabe kama huwezi kuomba radhi pale unapokosea.
Wewe ni dhaifu sana kama ujanja wako ni kudhulumu jasho la wenzio.
Wewe bado huna nguvu, kama kupanda kwako ni mpaka ushushe wengine.
Ushindi mkubwa wa maisha ni ule wa kuishinda nafsi yako mwenyewe.
AJIRA- Ni kitendo cha kwenda kuishi ofisini na jioni kurudi kutembea nyumbani kwa maisha yako yote ya ujana, kisha ukizeeka wanakwambia usije tena.
LIKIZO- ni ruhusa ya kutofika kazini anayopewa mtumishi kila mwaka ili kumkumbusha kuwa kampuni inaweza kuendelea kuwepo bila yeye.
Mavumbini, yupo baba aliyeleta hali na matumaini nyumbani.
Yupo mama, aliyekua anapoteza usingizi wake usiku wa manane kutuombea dua.
Mwisho, chini ya ardhi yupo boss aliyetuambia akitoka katika kitanda cha hospitali kila kitu kitakua shwari kuhusu ile kazi.
Kaburi..🙏
Mwambie huyo dada, tupo kwaajili ya kutatua majukumu yetu na sio tamaa zake..
Akitaka tumpeleke vacation Dubai, wakati uwezo wetu ni Zanzibar, hizo ni tamaa zake.
Akiingia period akahitaji pedi, akiumwa akahitaji hela ya matibabu, hayo ni majukumu yetu.
TAMAA VS MAJUKUMU YETU.
Mwanangu Castro, huwa ananiambia, MAFANIKIO YANANUNULIWA KAKA.
Kauli kali sana, yenye ukweli ndani yake..
Ili mafanikio yatokee, yakikosa bahati, kujuana, unauziwa na washika dau.
Juhudi ni kapaumbele, ila hakitoshi..
Zama hizi Connection zinauzwa..
Tusameheni mnaotupenda na hatuoneshi kujali,
Mnaotushirikisha vitu na bado tunajitenga,
Mnaotupa sikio na bado tunawaficha mambo yetu. Hatufanyi hivyo kwa kupenda.
Baadhi yetu tunahukumiwa na historia, tuliwahi kuwaamini watu wakatupakazia ubaya, na sasa tupo kama walivyotaka.
Utakutana na watu wenye vinywa safi lakini mioyo yao inanuka
Marafiki watakao lipia bill zote za baa, lakini hawatashika simu utakapopatwa na tatizo nje ya ulevi
Washikaji mtakao kwenda mezani kwaajili ya matumbo yenu.
Lakini hawatakusindikiza kaburini kwaajili ya mwisho wako.
Kama una mahusiano na dada yangu, ikatokea amekuumiza moyo wako..
Tafadhali, usimpe kiapo cha "Kaka yako na yeye yatamkuta kama uliyenitendea"
Mi sihusiki na ugomvi wenu, Msinihusishe..🙏